Vyombo vya habari vina nafasi kubwa ya kuhamasisha usawa wa uongozi.

 

Dk. Mzuri Issa ambaye ni Mkurugenzi Tamwa Zanzibar akizungumza na waandishi kabla ya kuwasilishwa utafiti uliolenga kuangalia vyombo vya habari jinsi wanavyotoa habari za wanawake huko katika afisi za taasisi hiyo Tungu Mkoa wa Kusini Unguja

Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Wanawake Tanzania, Zanzibar ( TAMWA, ZNZ)  DK. Mzuri Issa Ali amesema Vyombo vya habari vina nafasi kubwa ya  kuweka usawa wa kijinsia katika nafasi za uongozi kwa wanawake.

Dk. Aliyaeleza hayo Huko Tungu Mkoa wa Kusini Unguka katika afisi ya Tamwa, wakati akifungua mkutano wa uwandishi wa habari  na wadau  kutoka taasisi za habari na tasisi zinazoshughuika na utetezi wa wanawake ambapo kuliwasilishwa kwa ripoti ya Utafiti jinsi  vyombo vya habari vinavyoripoti habari za wanasiasa wanawake hapa nchini.

Alisema umefika wakati sasa vyombo vya habari kuandika habari ambazo zinaeleza umuhimu wa wanasiasa mwanamke katika majukumu yao ya  uongozi na pia kuelezea yale mazuri ambayo wanayoyafanya katika utendaji wao.

“Tukiandika habari za utendaji wa wanawake na umuhimu wao wa kushika uongozi katika siasa italeta hamasa kwa wanawake wengine  kuingia katika kugombania nafasi mbalimbali za uongo hizo” alisema Dr. Mzuri

Alisema lengo la kufikia 50 kwa 50 litaweza kufanikiwa ikiwa vyombo vya habari vitajikita katika kuandika habari za wanawake ambazo zitawatia hamasa za kugombea nafasi za uongozi kwa ngazi zote.

“Masuala ya uongozi ni matakwa ya Kitaifa na kimataifa mpaka 2030  tuwe tumefikia asilimia  50 kwa 50” alisema Dr. Mzuri.

Akiwasilisha Utafiti huo uliofanywa kwa kipindi cha miezi nne kutoka Januari ,Aprili, Juni na Agosti  2021 Dk Abubakar Rajab alisema kwamba kwa mujibu wa utafiti huo umegundua baadhi ya vyombo vya habari bado vina uchache wa habari zinazolenga  wanasiasa wanawake na uongozi.

Alisema habari nyingi za wanasiasa wanawake kuwa ni chache na hata hizo chache zimewekwa katika kurasa za ndani kuazia kurasa ya tano au kurasa za ndani zaidi.

Katika utafiti huo gazeti la mwananchi limeonekana kwa kiasi limeongeza kutoa taarifa juu ya wanawake na uongozi wa siasa kulikoni Zanzibar leo ambalo ni gazeti la serikali Visiwani Zanzibar.

Baada ya uwasilishwaji wa ripoti hiyo Mhariri Mtendaji Zanzibar leo Ali Haji Mwandini alionyesha kuguswa na kusema “Utafiti huu utatuwezesha Zanzibar leo kujipanga upya ili kuongeza kasi ya kutoa habari za jinsia ya kike na uongozi kwa upana zaidi” .

Kwa upande wake Muandishi Mkongwe Hawura Shamte alisema ni vyema utafiti mwengine ukaangalia na uwepo wa picha za wanasiasa  wanawake na uongozi kwani picha huwa zinatoa maelezo mengi kuhusiana na tukio.

“Picha ni nzuri sana inaweza kuleta mvuto mkubwa kwenye utafiti kwani picha moja inatoa ujumbe zaid ya maneno 1000 na maneno hayo yanaweza kuleta maana na tafsiri mbali mbali” alisema Hawura.

 

Mapema mkurugenzi wa chama cha waandishi wa habari wanawake Dk.Mzuri Issa amewataka waandishi wa habari kufanya kazi kwa kuzingatia maslahi ya jamii ya wanawake na kuona sauti zao zinasikika kupitia vyombo vya habari.

 

‘’Vyombo vya habari vyetu bado vinawajibikakwa kiasi kikubwa kutoa taarifa za jamii ya wanawake ili sauti zao ziweze kusika hatua ambayo itasaidia kupiga hatua za maendeleo kwa kuibuwa changamoto zinazowakabili’’amesema.

 

About mmedia

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment