Mbunge wa Jimbo la
Kikwajuni Alhaj Hamad Yussuf Masauni amekabidhi Magongo na Gharama za uwezekaji
wa Paa katika Chuo cha Madrasatul Ndamba iliyopo Miembeni Wilaya Mjini Unguja
Hatua ya kukabidhi
vifaa hivyo ni muendelezo wa utekelezaji wa Ahadi zake ikiwa ni sehemu ya Pili
ya ziara anazoendelea kuzifanya katika maeneo mbalimbali ya Jimbo hilo
Akiwa katika ziara hiyo
aliyoifanya Jana (Jumatatu 29 Novemba, 2021) aliongozana na Uongozi wa Chama
Cha Mapinduzi Jimbo la Kikwajuni Ukiongozwa na Mwenyekiti wa Jimbo hilo Nd
Mvita Kibendera pamoja na viongozi wengine wa kamati ya Siasa ya Jimbo
Alhaj Masauni amesema
atahakikisha anatumia uwezo wake wote kwaajili ya kutatua changamoto mbalimbali
zinazowakabili wananchi wa Jimbo hilo huku akitilia mkazo kwenye changamoto za
upatikanaji wa Elimu na uwezeshaji wananchi kiuchumi
"Heshima
muliyonipa Wananachi wa Kikwajuni ni kubwa mno na mimi nafanya yote haya
kwasababu ya heshima muliyonipa hivyo nitaendelea kutumia rasilimali zote ili
kuhakikisha nakabiliana na changamoto zinazowakabili hasa kwenye kusaidia
utoaji wa Elimu bora na Misingi ya kuwawezesha kujikwamua kiuchumi"
alisema Masauni
Akikubali ombi la kuwa
Mlezi wa Madrasa hiyo Alhaj Masauni amesema ipo haja kwa Uongozi wa Mfuko wa
Elimu wa Jimbo hilo kuzipitia madrasa zote zilizopo Jimboni ili kuweka mikakati
mbalimbali ya kuhakikisha zinafikiwa na fursa mbalimbali zitokanazo na Mfuko
huo aliyouanzisha kwa lengo la kusaidia harakati za Elimu ndani ya Jimbo
Aliwataka Uongozi wa
Madrasa hiyo pamoja na wananchi wote kubuni miradi mbalimbali ya Maendeleo
itayosaidia kuwaingizia kipato kwaajili ya kuendesha shughuli mbalimbali
"Natoa Rai kwa
Uongozi wa Madrsa lakini na kwa Wananchi wote wa Jimbo hili, tafuteni miradi
yenye tija ambayo yatawasaidia kiuchumi na mie nitakua tayari kuwawezesha ili
kufanikisha malengo hayo" alisema Masauni
Mapema Mwalimu Mkuu wa
Madrasa Damba Sheikh Mohammed Othman amemshukuru Mbunge wa Jimbo hilo kwa
kuwafikia na kuteleza ahadi hiyo hali itakayosaidia kwa kiasi kikubwa kumaliza
kwa ujenzi huo na kutatua changamoto ya uhaba wa eneo la kuwafundishia watoto
wa madrasa hiyo
Alifafanunua kuwa ipo
haja kwa wazazi kutoa Mashirikiano ya kutosha ikiwa ni pamoja na ulipaji wa ada
ili kusaidia uendeshaji wa Madrasa hiyo ikiwemo mishahara ya walimu
Katika Hatua nyengine
Mhandisi Masauni aliendelea na ziara katika eneo la Mpirani kuzungumza na
Wananchi wa eneo hilo na kusikiliza changamoto mbalimbali zinazowakabili
Alimalizia ziara yake
kwa kuwatembelea Wazee akiwemo Bi Attiy Salim Said katika makaazi yake yaliyopo
Miembeni Mjini Unguja
0 Comments:
Post a Comment