![]() |
| Waziri wa Ujenzi , Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar Rahma Kasim Ali |
Waziri wa Ujenzi Mawasiliano na Uchukuzi
Rahma Kassim Ali ameunda timu ambayo itaweza kufuatilia kwa karibu ujenzi wa
bandari ya mkokokotoni kwa kile kilichonekana kuwa bandari hiyo imekua
imechukua muda mrefu katika utekelezaji wake kinyume na makubaliano ya
awali wa mkataba wao baina ya serikali na mkandarasi.
Akizungumza katika ziara ya kukagua
ujenzi huo uliopangwa kukamilika mwezi huu wa septemba amesema hajaridhishwa na
hatua iliyofikiwa jambo linalochelewesha matumizi ya bandari hiyo hasa katika
fursa za kibiashara
Amesema uwepo wa timu hiyo
utafuatilia kwa karibu zaidi ujenzi ikiwemo kuangalia ubora wa ujenzi ili
kudumu kwa muda mrefu kwani imekuwa jambo la kawaida kwa wasimamizi wa ujenzi
kujenga kwa kutojali ubora kutokana na sababu za kuharakishwa.
Akizungumzia umuhimu wa bandari hiyo
waziri Rahma amesema itaweza kusaidia usalama wa wanaovuka kwenda kisiwa cha
tumbatu pamoja na kupunguza urefu wa masafa ya wanaosafiri kwenda pemba,tanga
na bagamoyo
Nae mkuu wa mkoa wa kaskazini unguja
Ayoub Mohammed Mahmoud amehimiza watendaji wa bandari kuanza matayarisho ya
ujenzi wa majengo yaliyo ncje ya mradi huo yakiwemo maeneo ya kuhudumia
watakaotumia bandari hiyo ikiwemo ofisi za kuuzia tiketi sehemu za huduma
za kijamii pamojab na vituo vya afya ili ujenzi utakapokamilika kuanza
kazi moja kwa moja.
Hata hivyo mkuu wa mkoa huyo
alimkumbusha wajibu wake msimamizi wa mradi huo ambao ni wakala wa majenzi Zanzibar
kusimamia vyema kwa kuhakikisha anapita
mara kwa mara ili kuhakikisha mradi huo unamalizika kwa wakati na kwa kiwango
kilichopangwa.
Aidha mhe ayoub amemtaka mkandarasi
huyo kuhakikisha muda wa miezi mitatu aliomba kutoka serikali ahakikishe
anajipanga vyema ikiwa ni kuongeza kwa vifaa na wafanyakazi ili aweze kwenda
sambamba na muda aliomba.
Kwa upande wa wananchi Ayoub
aliwatoa hofu wananchi wa mkoa huo kwamba serikali inaendelea na jitihada za
kuhakikisha mradi huo unamaliza kwa wakati na ifikapo januari bandari hiyo
itaanza kutumika
Akitaja sababu za kuchelewa kukamilika
kwa mradi huo injinia Ediel kimaro kutoka kampuni ya Edge
consultation .amesema imetokana upatikanaji wa mawe ulikua wa shida jambo
ambalo liliwafanya wakae miezi 2 bila ya kufanya kazi.
Aidha Mkandarasi huyo aliahidi
kumaliza kazi hiyo kwa muda aliomba na kwa sasa kazi hiyo imefika asilimia 75
ambapo alisema hivi sasa wanamalizia kazi ya ujazaji mawe na hivi punde
wataanza kazi ya uwekaji zege

0 Comments:
Post a Comment