Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent
Bashungwa amewataka wasanii wa Tanzania kutumia muda wao vizuri na kuachana na
malumbano, ili kupata muda wa kutengeneza kazi zenye ubora na mvuto kwa
watazamaji na wasikilizaji ambazo zitawanufaisha.
Bashungwa ametoa kauli hiyo leo Disemba 2,
2021 jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza katika hafla fupi
iliyoandaliwa na kampuni ya MultChoice Tanzania kuonesha mafanikio na mipango
yake katika Sekta ya Sanaa.
Aidha, amefafanua kuwa Serikali itaendelea
kuwawekea mazingira wezeshi katika kutimiza ndoto zao kupitia tasinia ya sanaa.
" Watanzania wanahitaji burudani zenye
mafundisho na zilizo andaliwa kwa kiwango kinacho ridhisha nashauri wasanii
kutumia muda wenu vizuri kuzalisha filamu au kutengeneza muziki unaokidhi
vigezo kwa ajili yenu na kwa ajili ya taifa". Amesema Mhe. Bashungwa
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya
Multchoice Tanzania Bi. Jacquiline Woisso ameishukuru Serikali kwa ushirikiano
mkubwa inaowapatia katika utendaji wa kazi zao za kila siku.
Aidha, Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania,
Dkt. Kiagho Kilonzo ameiomba Kampuni ya Multchoice Tanzania kupandisha
bei ya ununuzi wa filamu akisema baadhi ya wasanii hawako tayari kupeleka
filamu zao katika kampuni hiyo kwa madai kuwa gharama ya ununuzi wa filamu zao
bado ni ndogo ikilinganishwa na ubora na gharama kubwa zinazotumika kuandaa
filamu hizo.
Hafla hiyo fupi imeenda sambamba na uzinduzi wa
filamu mbili ambazo ni tamthilia ya Danga na la Familia.
0 Comments:
Post a Comment