SMZ Kuazisha shule maalum kwa ajili ya watu wenye ulemavu

 


MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Othman Masoud Othman, amesema kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekuwa ikifanya juhudi kubwa kusimamia maslahi ya Watu wenye Ulemavu katika nyanja tofauti  kwa nia ya kutoa fursa zaidi za maendeleo ikiwemo suala la elimu ya kuwajengea uwezo mkubwa zaidi.

 

 Othman ameyasema hayo leo huko Nungwi Wilaya ya Kaskazini ‘A’ Unguja alipozungumza katika maadhimisho ya kilele cha siku ya watu wenye ulemavu duniani ambazo kitaifa zimeadhimishwa leo hapa Zanzibar.

 

Makamu amesema kwamba kupitia wizara ya Elimu ya Zanzibar, Serikali imeanzisha mfumo wa shirikishi na mjumuisho wa elimu ili kuwapatia fursa kubwa za stadi za maisha sambamba na kutoa nafasi za ungozi kwa watu wenye ulemavu Zanzibar wa waina mbali mbali .

 

Amefahamisha kwamba katika jitihada za kuendelea kutoa fursa kwa watu wenye ulemavu hivi karibu ni serika.li ya mapinduzi ya Zanzibar itaanzisha ujenzi wa shule maalum jambo ambalo linaongeza juhudi katika kuongeza mslahi ya watu wenye ulemavu Zanzibar.

 

Aidha amesema kwamba serikali imeimarisha mazingira bora ya kusaidia na kushajiisha washirika wa maendeleo ili  kuwasaidia zaidi Watu Wenye Ulemavu jambo ambalo linakwenda sambamba na juhudi za dunia za kuwatetea watu wenye ulemavu kupitia  maazimio  mbali mbali ambayo yanaongeza nguvu katika kuingiza masuala ya watu wenye ulemavu katika masuala tofauti ya nchi.

 

Amesema Serikali ya Zanzibar kwa kushirikiana na Jumuiya ya kimataifa inaendelea na michakato  mbali mbali ya kuimarisha sera na sheria zinazosimamia maslahi ya Watu wenye ulemavu, jambo ambalo limesaidia sana kuanzishwa kwa Baraza la Watu wenye Ulemavu Zanzibar chombo ambacho nimuhimu katika kusimamia na kutetea haki zao.

Amesema kwamba serikali inajitihadi kuwa na sheria bora za kulinda maslahi ya au wenye ulemafu pamoja na kuweka mkazo mkubwa wa usimamizi wake ikiwa ni pamoja shuriki wa watu wenye ulemavu katika masuala ya siasa katika kuweka ushirikishwaji sawa kama haki yake ya kisiuasa sambamba kujengwa miundo mbinu rafiki kwa jamiii hiyo ili Zanzibar kuwa nchi ya mfano katika kulinda maslahi ya watu wenye ulemavu.

 

Aliwakumbusha Baraza , Viongozi na Jumuiya ya watu wenye ulemavu Zanzibar kujaandaa kuhesabiwa katika sense ijayo ya mwaka 2022 ambayo itasaidia kupaanga masuala mbali mbali ikiwemo maslahi ya watu wenye ulermavu .

 

Aidha aliwakumbusha kinamama kwenda hospitali mapema kuchunguzwa afanya za watoto na wale ambao watakuwa wamepata watoto wenye ulemavu atrhari za ulemavu zitaweza kupunguzwa iwapo wamewahishwa hospitali.

 

Pia Mhe. Othman amewataka wanajamii kuacha tabia iliyojengeka ya kusbabaisha ongezeko la ajali kwa ajali za barabarani zinazotokana na uzembe kwa kutozingatiwa ipasavyo kanuni na sheria za usalama barasbarani.

 

Naye Waziri wa Nchi Afisi ya Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Dk Saada Salum Mkuya Salum amsaema kwamba takwimu zinaonesha kuwa Zanzibar inaasilimia 5.8 ya watu wenye ulemavu wa aina mbali mbali  na takwimu hizo zinaoweza kuongezeka kwa kuwa watu wengi hawajajitokeza na taarifa zao kufahamika.

 

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kaskazi Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud amsema kwamba mkoa huo ulitajwa kwamba ulikuwa unaongoza katika takwimu za vitendio vya udhalilishaji lakini hivi sasa hgali hiyo imekuwa na mabadiliko makubwa .

 

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Watu Wenye Ulemavu Zanzibar Bibi Salma Saadat, amepongeza juhudi za serikalki katika kuhakikisha maslahi ya watu wenye ulemavu yanazingatiwa na kulindwa vyema na kuwataka wanajumuiya hizo kuhakikisha wanaongeza ushirikiano katika kudai haki zao mbali mbali.

 

Siku ya watu wenye ulemavu duniani huadhimishwa kila ifikapo Disemba tatu ya kila mwaka ambapo Ujumbe wa mwaka huu ni “Uongozi na Ushirikishwaji wa Watu wenye ulemavu kuelekea ujumuishwaji na ufikiwaji endelevu baada ya uviko 19  

About mmedia

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment