Suzan awassshauri Wavuvi kuazisha vikundi

 

Mkuu wa Wilaya ya magharibi B Unguja Suzan Kunambi akizungumza na wavuvi katika Diko la Mtoni Kigomeni

Mkuu wa Wilaya ya Magharibi A Bi. Suzan Peter Kunambi ameshauri  Wavuvi kujiunga katika vikundi ili kufanya kazi zao kwa mashirikiano lakini pia iwe rahisi kupata fursa zinazotolewa na Serikali ikiwemo mikopo.

Ameyasema hayo huko  Katika diko la Mtoni Kigomeni  alipokuwa akizungumza na Wavuvi  wa eneo hilo ,kwa lengo la kuwahamasisha kuanzisha vikundi vya ushirika.

Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeandaa program maalum ya uwezeshaji wananchi kiuchumi na wavuvu ni moja kati ya kundi yatakaonufaika na mpango huo hivyo ni vema kuwa tayari  kwa kufuata mashariti kwani  watakaonufaika na fursa hiyo ni wale watakao kuwa wamesajiliwa rasmi .

Amefahamisha kuwa mikopo hiyo haitakuwa na riba masharti magumu itatolewa kupitia fedha za IMF Uviko 19.

Mkuu huyo wa Wilaya amezitaja fursa zinazotarajiwa kutolewa na Serikali kupitia Wizara ya Uchumi wa bluu ni pamoja na kuwapatia wavuvi  boti zenye mashine na zana zote za uvuvi na mafunzo maalum ya teknologia bora ya uvuvi.

 Dhamira ya Serikali ni kuleta mageuzi makubwa katika shughuli zote zinazofanywa na Wavuvi wa maji madogo lakini pia katika eneo la bahari kuu ili kupata  maendeleo ya haraka na kuimarisha Uchumi wa bluu nchini .

Amewasisitiza kwa wale watakaobahatika kupata mikopo hiyo kuitumia vizuri na kuirudisha kwa wakati ili na wengine wanufaike.

Wakitoa changamoto zao kwa pamoja Wavuvi hao wamesema,Miundombinu ya Mabanda wanayotumia kwa sasa hayaridhishi pamoja na kukosekana kwa huduma ya Maji safi na Salama na huduma ya vyoo katika Eneo hilo imekuwa ni changamoto inayowapelekea usumbufu katika Shughuli zao.

Aidha wameiomba Serikali kuwapatia ufumbuzi kwa haraka kwa vile maji na huduma ya choo ni muhimu katika mikusanyiko ya watu.  

Aidha wametoa  shukurani zao kwa  Mkuu huyo  wa Wilaya kwa  kufika katika eneo hilo kuwaelimisha na kuwaeleza dhamira njema ya Serikali kwao.

 Wamesema wamefurahishwa na ujio wa Mkuu huyo katika eneo lao kwani  amejionea mwenyewe  Mazingira magumu  na hali halisi  wanayopitia wavuvi hao .

Wamesema  Imani yao kwa Serikali ya  Wilaya ni watapatiwa ufumbuzi kwa haraka wa changamoto zao

Akijibu kuhusu changamoto zilizotolewa na wavuvu hao Mkuu huyo amewataka Wavuvi hao kuwa na subra katika kipindi hichi,kwani   Serikali  kupitia Manispaa ya Magharibi A Ina mpango wa kuboresha eneo hilo kwa   kujenga Mabanda ya uhakika na ya  kisasa ili kuwafanya wavuvi hao wafanye shughuli zao katika mzingira mazuri.

About mmedia

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment