Mchezaji Othman Miraji Bingwa Judo Zanzibar katika ngazi ya miaka 6 na 14







MCHEZAJI Othman Miraji ameibuka na ubingwa wa michuano ya Judo ya watoto yaliyofanyika katika ukumbi wa Chama Cha Judo uliopo Amaan mjini Unguja.

 

Mashindano hayo ya siku mbili yaliandaliwa na chama cha mchezo huo na kushirikisha watoto kuanzia mika sita hadi 14.

 

Katika mashindano hayo bingwa alikabidhiwa medali ya dhahabu, cheti cha ushiriki na baskeli, wakati nafasi ya pili iliyokwenda Haris Mohamed alipata medali ya fedha, cheti na rice cooker.

 


Zawadi ya mshindi wa tatu ambayo ni medali ya shaba, cheti na Electric kettle, ilichukuliwa na washiriki watatu ambao ni Lukman Abdulla, Mbarouk Farouk na Abdillah Mgeni.

 

Mashindano hayo yaliyofanyika Novemba 28 mwaka huu, yalishirikisha wachezaji 53 kutoka maeneo mbali mbali mbali ya ya Zanzibar, ambapo na kupatiwa zawadi washindi lakini washiriki wote walipatiwa fulana.


About mmedia

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment