Zaidi ya wanachama
wapya 250 wamejiunga na chama cha ACT
Wazalendo na kupokewa na Mwanasheria
mkuu wa cha hicho Omar Said Shabaan.
|
Shaaban aliwapokea
wanachama hao huko Kwa Maharouk Jang’ombe Jimbo la mpendae katika shuhuli iliotayarishwa
na Ngome ya wanawake ya chama hicho. Akizungumza katik
shuhuli hiyo Shaabani aliwapongeza viongozi wa ngome hiyo kutokana na kazi
kubwa wanaiyoifanya ambayo matunda yake yanaonekana. Alisema kazi ya
kuwapata wanachama 250 wakajiunga na chama hicho ni kazi ngumu na ya kupigiwa
mfano, na kutokana na kazi hiyo aliwapatia zawadi ya laki tatu kwa juhudi zao. Sambamba na hilo
Shaaban aliwaambia wanachama hao kujisikia kama wao wamejiunga na chama hicho
muda mrefu kwani wana haki sawa na wengine Mapema Mwenyekiti timu
Mkakati ya Ngome hiyo Pavu Abdallah allisema wanachama hao walikuwa nao katika
chama cha CUF lakini walipohama wao waliobakia huko. “Lakini leo wameamua
kujiunga katika Juhudi za kupigania uwepo wa Zanzibar yenye mamlaka kamili na
tunawaambia karibuni tuendeleze mapambano” alisema Pavu. |
0 Comments:
Post a Comment