Kamati ya Baraza la Wawakilishi yataka usiamizi bora mradi wa mitaro Pemba





 Kamati ya bajeti  ya baraza la wawakilishi Zanzibar  imeitaka ofisi ya makamu wa kwanza  wa  Rais   Pemba pamoja na idara zake  kuhakikisha wanaendelea kusimamia maradi wa uimarishaji wa  msingi wa maji taka katika mji  ili uweze kukamilika  kwa wakati .

Kauli  hiyo imetolewa na  mwenyekiti wa kamati hio Ali Suleiman Ameir  mara  baada  ya  kutembelea  na kukagua mradi wa uimarishwaji   mfumo  wa  maji taka huko katika eneo la Msingini na Kichungwani katika mji wa  chake chake  mkoa wa kusini pemba.

Alisema  endapo  ofisi hiyo pamoja na idara zake  utasimamia  mradi huo matokeo chanya yatapatikana   baada ya kukamilika mradi huo .

"Ombi langu kwa ofisi ya makamu wa kwanza wa rais na idara zake lakini pia idara za  mazingira na usimamizi  wa mazingira ikiwemo zema  kuendelea kusimamia  mradi huu ili matokeo chanaya mwisho wa mradi huu yaweze kukamilika" alisema  .

Hata hivyo mwenye kiti huyo aliwataka wananchi ambao watatumia   moja kwa moja mradi huo  kuupokea mradi huo na kuutumia kwa uanagalifu ikiwemo kuitunza ili iweze kudumu kwa muda mrefu.

 Kwa upande wake katibu mkuu wa  ofisi  ya makamu wa kwanza wa rais  Omar Dadi Shaka   alisema  kuwa bado wananchi wamekuwa na uelewa mdogo juu ya atahari za mabadiliko ya tabia ya nchi  jambo ambalo hupelekea  kurudisha nyuma juhudi zinazofanywa na serikali katika kuimarisha mazingira   siku hadi siku

Ipo haja ya kutanua wigo  wa kushughulikia masuala ya mazingira  ili kuleta maendeleo na kuimarisha miji kiasili  katika kutunza na kuhifadhi mazingiara na kupunguza hali ya joto na mabadilko ya tabia  nchi  katika makazi ya watu.

Ziara hiyo ya kukagua mradi huo wa majitaka  ilianzia  katika shehia  msingini  Afrikana na kumalizia    banda taka kichungwani  .

About mmedia

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment