![]() |
| Waziri wa Nchi wa Afisi ya Makamu wa kwanza Rais Zanzibar Sada Mkuya Salum. |
Raya Hamad – 0MKR
Waziri
wanchiOfisiwaMakamuwa Kwanza wa Rais Dkt. Saada Mkuya Salum
amefanya uteuzi wa wajumbe wa Baraza la Taifa la Watu wenye Ulemavu kwa kipindi
cha miaka mitatu 2021 – 2023.
“Kwa
mujibu wa Sheria ya Watu wenye Ulemavu (Haki na Fursa) Namba 9 ya Mwaka 2006, Waziri
wa nchi Ofisi ya Makamuwa Kwanza wa Rais amewateua wafuatao kuwa wajumbe wa Baraza
la Taifa la WatuWenyeUlemavu”
Aliowateua
ni Mohammed Abdallah Mohammed – kutoka Jumuiya ya Watu wenye Ualbino Zanzibar
(JMZ), Nassor Suleiman Nassor kutoka Umoja wa Watu wenye Ulemavu Zanzibar
(UWZ).
Kwa
upande mwengine waziri Mkuya aliwateuwa Afwa
Nassor Hassan – kutoka Chama Cha Viziwi Zanzibar (CHAVIZA) sambamba na Fatma Djaa
Chesa – kutoka Jumuiya ya Watu Wasioona Zanzibar (ZANAB).
Pia Waziri huyo alifanya utuzi kwa HidayaMjaka Ali – kutoka Jumuiya ya Wanawake wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA), Pamoja na HaroubSoudMzee – kutokaKituo cha Watu wenye Ulemavu na Maendeleo Jumuishi Zanzibar (ZACEDID).
Kwa upande jumuiya ya waajiri na chama cha wafanyakazi Zanzibar pia aliwateuwa Mohamed Najim Omar – kutokaJumuiya cha Waajiri Zanzibar (ZANEMA), na Sharifa Mohamed Salum – kutoka Chama cha Wafanyakazi Zanzibar (ZATUC).
Uteuzi huu ni kufuatia Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi,
kumteuwa Salma Saadati Haji kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Watu wenye Ulemavu
tarehe18 Agosti, 2021.
Uteuzi wa Wajumbe wa Baraza
la Taifa la Watu wenye Ulemavu, unaanza tarehe 01 Oktoba, 2021.

0 Comments:
Post a Comment