TAFAKURI Nani anayeruhusu ujenzi mikokoni Mpigaduri?

 




Salum Vuai Issa9Muhenga)
 

Salum Vuai

 

MIAKA kadhaa iliyopita, mimi na mpiga picha wangu tuliwahi kulitembelea eneo la Mpigaduri karibu na skuli ya maandalizi Saateni Wilaya ya Mjini.

 

Wakati huo ndio kwanza watu walikuwa wameanza kulivamia eneo hilo na kukatiana au kugaiana viwanja kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za makaazi.

 

Katika hali ambayo hatukuitarajia, tulikuta mikoko mingi imekatwa kupisha ujenzi wa nyumba za tofali tena zilizoezekwa bati kama kwamba eneo hilo limehalalishwa na mamlaka zinazosimamia ardhi nchini.

 

Tulipiga picha nyingi na kuzitumia katika gazeti la Zanzibar Leo kwa lengo la kuziamsha mamlaka zenye dhamana ya ardhi, mipango miji na mazingira tukiamini pengine hazikuwa na habari juu ya kinachoendelea mikokoni humo.

 

Kumbe kitendo hicho hakikusaidia chochote na niseme tu ilikuwa kama tumewachonga watu ukali.

 

Watu waliendelea kujimilikisha maeneo hayo hadi yakageuka mtaa mpya, ambao bila shaka unapata baraka zote za taasisi nyengine kwani  huduma za umeme na maji zinapelekwa na watu wanaishi raha mustarehe.

 

Kwa hakika hii inashangaza kwani katika hali ya kawaida, Tafakuri isingetarajia watu wakatiwe viwanja, kujenga nyumba na kuanzisha makaazi kwenye maeneo hayo.

 

La kushangaza zaidi, haya yanafanyika katika eneo ambalo liko karibu kabisa na idara ya Mazingira Maruhubi. Je, wahusika hawana habari?

 

Kwa watu wenye umri kuanzia miaka 50 na kuendelea ambao wanalijua vyema eneo hilo na mitaa inayolizunguka, watakuwa wanaelewa vyema kwamba katika miaka ya nyuma sehemu hiyo ilikuwa na mandhari nzuri kwa vile maji ya bahari yalipojaa yalifika hadi huko kulikojengwa sasa.

 

Sote tunafahamu kuwa, endapo mtu anahitaji ardhi kwa ajili ya ujenzi, anapaswa kufuata taratibu za kisheria kwa kupitia ngazi husika zinazohusisha halmashauri za miji, masheha na Idara ya Ardhi na Upimaji.

 

Lakini kwa hali inavyoonekana, eneo hilo, ama watu wanajichukulia tu kama matunda pori yasiyokuwa na mwenyewe baada ya kuzungumza vizuri au wanauziana kinyume na sheria.

Yumkini haya yana mkono wa wenye dhamana ambao nao bila shaka wananufaika kwa njia moja au nyengine.

 

Ujenzi huu ni tishio kubwa la kimazingira katika kipindi hichi ambacho binadamu anaendeshwa zaidi na utashi wa nafsi yake, na kamwe hafikirii athari zinazoweza kutokea kwa nchi endapo atapuuza umuhimu wa kutunza mazingira na rasilimali za taifa.

 

Kwa hili, ndipo ninapoona kuwa tatizo la uharibifu wa mazingira halitokani na kile kinachoitwa mabadiliko ya tabianchi, bali husababishwa na 'Tabiawatu'.

 

Wakati viongozi mbalimbali pamoja na wanaharakati wa masuala ya mazingira, wakiendelea kufanya mikutano na warsha za kila mara zinazogharimu fedha nyingi, kujadili na kuweka mikakati ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi, wanasahau kwamba kinachotuumiza ni tabia za watu wasiojali na ambao hawataki kubadilika.

 

Ni kweli kwamba mabadiliko ya hali ya hewa yamekuwa yakisababisha athari nyingi katika jitihada za binadamu kujitafutia maendeleo, lakini kiumbe huyo huyo ndiye sababu ya majanga hayo.

 

Kwa kuwa utashi wa binadamu ndio unaowafanya wavamie rasilimali na maliasili za baharini na misituni na kuzihujumu, iko haja kwa wataalamu wa mazingira, walione pia tatizo la ‘TABIAWATU’.

 

Viongozi, wanaharakati na wadau wa mazingira wataendelea kupiga kelele kwa kulaumu tabianchi, lakini wafahamu kuwa, mikono ya watu ndiyo adui mkubwa wa janga la kimazingira linalozinyemelea nchi zetu hasa hapa Zanzibar.

 

Kama sheria za kulinda na kuhifadhi mazingira zipo, kwa nini watu wanazivunja na wanaonekana lakini hakuna hatua zinazochukuliwa dhidi yao?

 

Bila shaka, wanaovunja sheria hizo, wanapata jeuri kwa kuwa wanabebwa na kukingiwa kifua na baadhi ya watendaji wa ngazi za juu waliopewa dhamana ya kuzisimamia.

 

Kumbe tulikuwa tunasubiri ziara ya kiongozi wa juu katika eneo hilo ndipo waliopewa dhamana wazinduke na kujua athari inayoitafuna nchi?

 

Tutarajie ziara ya Makamu wa Pili wa Rais huko Mpigaduri iwe chanjo ya kinga ya uzembe na utendaji kazi kimazoea ili wananchi wasivuke mipaka ya uhuru walionao kwa kulazimisha mambo yasiyostahili yanayoweza kuipeleka nchi katika janga na majuto ya milele.

 

Tuache kuangalia pale tulipoangukia, badala yake tutazame wapi tulipojikwaa na kuchukua hatua muafaka kwa kubaini vyanzo vya matatizo yanayoimaliza nchi yetu, ambavyo kukabiliaana navyo kunahitaji zaidi vitendo na sio mdomo mtupu.

 

Simu: 0777 865050/0714 425556

Baruapepe: salumss@yahoo.co.uk.

 

Salum Vuai

 

MIAKA kadhaa iliyopita, mimi na mpiga picha wangu tuliwahi kulitembelea eneo la Mpigaduri karibu na skuli ya maandalizi Saateni Wilaya ya Mjini.

 

Wakati huo ndio kwanza watu walikuwa wameanza kulivamia eneo hilo na kukatiana au kugaiana viwanja kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za makaazi.

 

Katika hali ambayo hatukuitarajia, tulikuta mikoko mingi imekatwa kupisha ujenzi wa nyumba za tofali tena zilizoezekwa bati kama kwamba eneo hilo limehalalishwa na mamlaka zinazosimamia ardhi nchini.

 

Tulipiga picha nyingi na kuzitumia katika gazeti la Zanzibar Leo kwa lengo la kuziamsha mamlaka zenye dhamana ya ardhi, mipango miji na mazingira tukiamini pengine hazikuwa na habari juu ya kinachoendelea mikokoni humo.

 

Kumbe kitendo hicho hakikusaidia chochote na niseme tu ilikuwa kama tumewachonga watu ukali.

 

Watu waliendelea kujimilikisha maeneo hayo hadi yakageuka mtaa mpya, ambao bila shaka unapata baraka zote za taasisi nyengine kwani  huduma za umeme na maji zinapelekwa na watu wanaishi raha mustarehe.

 

Kwa hakika hii inashangaza kwani katika hali ya kawaida, Tafakuri isingetarajia watu wakatiwe viwanja, kujenga nyumba na kuanzisha makaazi kwenye maeneo hayo.

 

La kushangaza zaidi, haya yanafanyika katika eneo ambalo liko karibu kabisa na idara ya Mazingira Maruhubi. Je, wahusika hawana habari?

 

Kwa watu wenye umri kuanzia miaka 50 na kuendelea ambao wanalijua vyema eneo hilo na mitaa inayolizunguka, watakuwa wanaelewa vyema kwamba katika miaka ya nyuma sehemu hiyo ilikuwa na mandhari nzuri kwa vile maji ya bahari yalipojaa yalifika hadi huko kulikojengwa sasa.

 

Sote tunafahamu kuwa, endapo mtu anahitaji ardhi kwa ajili ya ujenzi, anapaswa kufuata taratibu za kisheria kwa kupitia ngazi husika zinazohusisha halmashauri za miji, masheha na Idara ya Ardhi na Upimaji.

 

Lakini kwa hali inavyoonekana, eneo hilo, ama watu wanajichukulia tu kama matunda pori yasiyokuwa na mwenyewe baada ya kuzungumza vizuri au wanauziana kinyume na sheria.

Yumkini haya yana mkono wa wenye dhamana ambao nao bila shaka wananufaika kwa njia moja au nyengine.

 

Ujenzi huu ni tishio kubwa la kimazingira katika kipindi hichi ambacho binadamu anaendeshwa zaidi na utashi wa nafsi yake, na kamwe hafikirii athari zinazoweza kutokea kwa nchi endapo atapuuza umuhimu wa kutunza mazingira na rasilimali za taifa.

 

Kwa hili, ndipo ninapoona kuwa tatizo la uharibifu wa mazingira halitokani na kile kinachoitwa mabadiliko ya tabianchi, bali husababishwa na 'Tabiawatu'.

 

Wakati viongozi mbalimbali pamoja na wanaharakati wa masuala ya mazingira, wakiendelea kufanya mikutano na warsha za kila mara zinazogharimu fedha nyingi, kujadili na kuweka mikakati ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi, wanasahau kwamba kinachotuumiza ni tabia za watu wasiojali na ambao hawataki kubadilika.

 

Ni kweli kwamba mabadiliko ya hali ya hewa yamekuwa yakisababisha athari nyingi katika jitihada za binadamu kujitafutia maendeleo, lakini kiumbe huyo huyo ndiye sababu ya majanga hayo.

 

Kwa kuwa utashi wa binadamu ndio unaowafanya wavamie rasilimali na maliasili za baharini na misituni na kuzihujumu, iko haja kwa wataalamu wa mazingira, walione pia tatizo la ‘TABIAWATU’.

 

Viongozi, wanaharakati na wadau wa mazingira wataendelea kupiga kelele kwa kulaumu tabianchi, lakini wafahamu kuwa, mikono ya watu ndiyo adui mkubwa wa janga la kimazingira linalozinyemelea nchi zetu hasa hapa Zanzibar.

 

Kama sheria za kulinda na kuhifadhi mazingira zipo, kwa nini watu wanazivunja na wanaonekana lakini hakuna hatua zinazochukuliwa dhidi yao?

 

Bila shaka, wanaovunja sheria hizo, wanapata jeuri kwa kuwa wanabebwa na kukingiwa kifua na baadhi ya watendaji wa ngazi za juu waliopewa dhamana ya kuzisimamia.

 

Kumbe tulikuwa tunasubiri ziara ya kiongozi wa juu katika eneo hilo ndipo waliopewa dhamana wazinduke na kujua athari inayoitafuna nchi?

 

Tutarajie ziara ya Makamu wa Pili wa Rais huko Mpigaduri iwe chanjo ya kinga ya uzembe na utendaji kazi kimazoea ili wananchi wasivuke mipaka ya uhuru walionao kwa kulazimisha mambo yasiyostahili yanayoweza kuipeleka nchi katika janga na majuto ya milele.

 

Tuache kuangalia pale tulipoangukia, badala yake tutazame wapi tulipojikwaa na kuchukua hatua muafaka kwa kubaini vyanzo vya matatizo yanayoimaliza nchi yetu, ambavyo kukabiliaana navyo kunahitaji zaidi vitendo na sio mdomo mtupu.

 

Simu: 0777 865050/0714 425556

Baruapepe: salumss@yahoo.co.uk.

About mmedia

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment