Picha za MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi akitembelea Maonyesho ya wajasiriamali Wilaya mjini

MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi akisalimiana na Viongozi wa UWT  alipowasili katika viwanja vya Kituo cha Amali Miembeni kuhudhuria Maadhimisho ya Wiki ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) yaliofanyika katika Kituo hicho, na (kulia kwake) Makamu Mwenyekiti wa UWT.Mhe Thuwaiba Editon Kisasi.(Picha na Ikulu)

MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi akimsikiliza Mjasiriamali wa Kikundi cha Chuo cha Wajasiriamali Wilaya ya Mjini kinachojishughulisha na utengenezaji wa losheni Bi. Rauhiya Abdalla Khamis, wakati akitembelea maonesho ya Wajasiriamali Wanawake wa Wilaya ya Mjini Unguja katika Maadhimisho ya Wiki ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) yaliofanyika katika viwanja vya Kituo cha Amali Miembeni na (kulia kwake) Makamu Mwenyekiti wa UWT Mhe Thuwaiba Editon Kisasi.(Picha na Ikulu).


 

About mmedia

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment