Jumla ya wanafunzi elfu moja miamoja na kumi na nane kati ya wanafunzi Elf saba miasita ambao waliripotiwa kukatisha masomo kwa utoro katika wilaya ya micheweni mkoa wa kaskazini pemba tayari wameanza kurudi katika skuli zao katika maeneo mbali mbali ya wilaya hiyo.
Akizungumza na habari hizi mkuu wa wilaya ya micheweni Mgeni khatib Yahya amesema juhudi hizo ni mashirikiano yake na wizara ya elimu kisiwani pemba katika kulisimamia suala hilo kwa wanafunzi hao.
Amesema kuwa idadi hiyo itaendelea kuongezeka siku hadi siku mpka pale watakaporejea wanafunzi wote kwani tayari wizara ya elimu inafuatilia suala hili ili kufanikisha taratibu za watoto hao kurudi skuli.
Alieleza kuwa wimbi hilo la wanafunzi ambao walikuwa hatarini kukatisha masomo kutokana na utoro lilisababishwa na sababu mbali mbali ikiwemo ajira za watoto katika wilaya hiyo, ambapo tayari uongozi wa wilaya unaendelea kulidhibiti suala haraka katika maeneo mbali mbali ya wilaya hiyo.
Aidha ameeleza kuwa wilaya hiyo imejiwekea mikakati madhubuti ili kuona watoto wote wanapata haki yao ya msingi ya kupata elimu kwa wale ambao wamekatisha masomo na wale ambao hawajaandikishwa waweze kupata haki yao ya lazima
Alieleza kuwa serikali ya wilaya tayari imeanza kuwapa onyo wale wote ambao wanatoa ajira kwa watoto ikiwemo kuwaanikisha madagaa, kupara samaki ndani ya Bandari kuacha mara mija tabia hiyo hatarishi kwa watoto.
0 Comments:
Post a Comment