Makamu wa Pili Aitaka Sekta ya utalii kubuni Mbinu Mpya za kuvutia Watalii

 


Makamu wa Pili wa Rais Hemed Suleiman Abdallah


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdullla amewataka wadau wa sekta ya utalii kubuni mbinu mpya zitakazosaidia kuwavutia watalii kurudi tena kuitembelea Zanziba
r.

 

Mhe. Hemed alitoa witò huo wakati akilifungua kongamano la wadau wa utalii Zanzibar lililofanyika katika Hotel ya Golden Tulip Airport Zanzibar.

 

Aliwashauri wadau hao kubuni mbinu mpya zenye kuzingatia ushindani kwa kuibua vivutio vipya sambamba na kuviimarisha vivutio vyengine ili viwe na mazingira yatakayowashawishi watalii kurudi tena kuitembelea Zanzibar.

 

Makamu wa Pili wa Rais aliwaomba wadau wa utalii kutorizike na dhana kuwa Zanzibar inajitangaza yenyewe bali inapaswa kuchukua jitihada za maksudi ili kuingia katika ushindani kutokana na nchi nyengine kuendelea kuchukua hatua mbali mbali za kutangaza nchi zao.

 

Aidha, Mhe. Hemed aliupongeza uongozi wa Jumuiya ya Kitaifa ya wafanyabiashara Zanzibar kwa kushirikiana na UNDP kwa hatua wanazozichukua katika kurudisha ustawi wa sekta ya utalii Zanzibar kwa ajili kuinua uchumi wa Nchi.

 

Alisema sekta ya utalii Zanzibar iliathiriwa na maradhi ya UVIKO-19 ambapo ikekuwa ikitegemea kwa asilimia kubwa ya ukuaji wa uchumi wake kupitia sekta ya hiyo.

 

Alieleza kuanguka kwa Soko la utalii Zanzibar kulipelekea kusimama kwa ajira nyingi za wanachi kulikosababishwa na kufungwa kwa hotel jambo lililopelekea kushuka kwa pato la serikali kwa ajilibya kutoa huduma msingi kwa wananchi wake.

 

"Athari za UVIKO-19 kumesababisha kushuka kwa ukushanyaji wa mapato jambo lililoathiri utoaji wa Huduma kama vile maji safi, ukarabati wa miundombinu ya Barabara" Alieleza Mhe. Hemed

 

Pamoja na mambo mengine Makamu wa Pili wa Rais alikemea vikali tabia inayofanywa na baadhi ya watembeza watalii kwa kuharibu viumbe hai vya baharini ikiwemo STAR FISH hali inayopelekea kuharibu rasilimali za bahari.

 

Nae, Waziri wa Utalii na mambo yakale Mhe. Lela Mohamed Mussa alisema wizara imekuwa na utamaduni wa kushirikiana na wadau tofauti katika kufufua utalii ulioathiriwa na maradhi ya UVIKO-19.

 

Alieleza kuwa, kutokana na maradhi ya UVIKO-19 kuikumba dunia imesababisha Jumuiya za kikanda ikiwemo Afrika Mashariki na SADC kuwa na vikao vya pamoja katika kujadili na kutathmini namna bora ya kufufua utalii katika nchi zake.

 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya kitaifa ya wafanyabiashara Zanzibar Ali Amour alimueleza Makamu wa Pili wa Rais kuwa katika mwaka 2020 sekta ya utalii ilitarajiwa kuchangia pato la taifa (GDP) kwa asilimia Thelasini na Tano (35%) pia ilitarajiwa kukusanya asilimia Themanini (80%) ya mapato pamoja na kuajiri watu wapatao laki moja (100,000) lakini kutokana na janga la UVIKO-19 lilisababisha kushindwa kufikiwa kwa lengo hayo.

 

Nae, Mwakilishi kutoka UNDP Madam Rukia Wadoud alisema UNDP inaipongeza serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa ushirikiano wake inautoa kwa kuwashirikisha wadau kutoka taasisi binafasi na kuahidi kuwa UNDP itaendelea kutoa ushirikiano wake kwa serikali ili kuinua maendeleo ya sekta ya utalii Zanzibar.

About mmedia

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment