Kuna kila Sababu ya kumuunga Mkono Mama Samia------ Mke wa Makamu wa Pili Zanzibar

 




Mama Sharifa Omar Khalfan akiwawashajihisha wanawake wa UWT Mkoa wa Kusini Unguja kuunga mkono Kauli ya Mama Samia ya kumuweka madarakani Rais mwanamke ifikapo 2025 wakati akizungumza katika hafla ya kupokea matembezi ya kumuunga Mkono Rais Samia yaliofanyika Mkoa wa Kusini Unguja.


Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Sharifa Omar Khalfan amesema kuna kila sababu ya kumuunga mkono Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan juu ya azma alionayo ya kuimarisha  uchumi wa Nchi.

Mama Sharifa Omar alieleza hayo katika kilele cha matembezi ya mshikamano ya kumuunga mkono mwenyekiti wa CCM ambae pia ni Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan mataembezi ambayo yaliyoanzia kibuteni na kumazia kizimkaazi Mkoa wa Kusini Unguja.

Mama sharifa alieleza kuwa, wanachama wa chama cha Mapinduzi na wananchi kwa ujumla wana kila sababu ya kumuunga mkonoi Rais Samia  kwa kazi kubwa anayoendelea kuifanya ya kuiongoza nchi ikizingatiwa kasi alioanza nayo ya kuwaeletea maendeleo wananchi wa Tanzania ndani ya kipindi cha muda mfupi.

Aidha, mke huyo wa  Makamu wa Pili wa Rais alisema ipo haja ya umoja wa wanawake mkoa wa kusini kuungana Pamoja na  kauli ya mwenyekiti wa CCM taifa ya kumuweka madarakani mwanamke kuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ifikapo mwaka 2025.

Pamoja na mambo mengine Mama Sharifa Khalfan aliwaeleza Umoja wa wanawake Mkoa wa Kusini kuwa  Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dk. Hussein Mwinyi anawaunga mkono na anawataka wanachama katika Mkoa huo kufanya kazi kwa umoja na mshikamano ili kuweza kuiletea maendeleo Zanzibar na Tanazania kwa Ujumla.

Akisoma risala ya Umoja wa wanawake wa Mkoa wa kusini Unguja katibu wa UWT wa Mkoa huo  Asha Mzee Omar  amesema uongozi wa UWT  Mkoa wa Kusini umeona ipo haja ya kuuanda matembezi hayo yenye azma ya kumpongeza mwenyekiti wa chama Taifa kutokana na  mwanzo mzuri wa utendaji wa kazi zake kwa kuisimamia demokrasia na  kuwajali wananchi wanyonge.

Aidha Katibu Asha amesema kuwa, kufuatia fedha zililizoelekezwa na mwenyekiti wa chama cha mapinduzi ambae pia ni Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia suluhu Hassan katika ngazi zote za halmashauri zitasaidia kwa kiasi kikubwa kuimarisha miundombinu yan chi sambamba na kupambana na maradhi ya UVIKO-19.

Nae  Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Kusini Unguja Shemsa Abdalla Ali amemuelezea Rais Samia kuwa ni kiongozi mwenye maono na kipaji cha uongozi kutokana na umahiri wake ndani ya kipindi cha muda mfupi ameanza kuonesha dira na mueleko chanya wa taifa la Tanzania.

Katika Hatua nyengine Mwenyekiti Shemsa Abdalla ametumia fursa hiyo kwa kuwashajihisha wanachi kuendelea kujitokeza kwa wingi kupata chanjo  ili kujikinga na maradhi ya UVIKO- 19 ambayo yamekuwa tishio Tanzania na duniani kwa ujumla.

Mapema Mama Sharifa Omar Khalfan amepokea matembezi ya kumuunga Mkono Mwenyekiti wa CCM Taifa Samia Suluhu Hassan yalioanzia Kibuteni na kumalizia Kizimukazi.

About mmedia

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment