| Salum Vuai |
Salum Vuai
“Kwa pamoja
tunaweza kuikoa dunia dhidi ya maafa”. Hii ni kaulimbiu ya maadhimisho ya Siku
ya Maafa Kimataifa ambayo iliadhimishwa jana Oktoba 13, duniani kote.
Maadhimisho ya
siku hii ni utekelezaji wa Azimio Na. 64/200 lililopitishwa na Baraza la Umoja
wa Mataifa tarehe 21 Disemba, 2009.
Siku hii
inalenga kukuza utamaduni wa usimamizi wa maafa kimataifa, ikiwa ni pamoja na
kuzuia, kupunguza madhara, kujiandaa, kukabili na kurejesha hali katika ubora
zaidi pale maafa yanapotokea.
Katika
kuadhimisha siku hii, Sekretarieti ya Upunguzaji wa Madhara ya Maafa ya Umoja
wa Mataifa (United Nation Strategy for Disaster Reduction–UNISDR) hutoa
kaulimbiu ya mwaka husika.
Katika tafakuri
yake wiki hii, Muhenga anauliza je, ni wangapi wako tayari kushirikiana na
wengine kwa kutoa mchango wa dhati katika kuhakikisha dunia inakuwa mbali na
maafa?
Yumkini
wanaotaka mafanikiio katika hili ni watu wote katika kila nchi, lakini wasiwasi
wa Muhenga ni kwamba miongoni mwao wapo wasiokuwa na dhamira ya kweli katika
kuifanya dunia iwe pahala salama pa kuishi.
Bila shaka wapo
wanaoangalia zaidi masahi yao binafsi kwa tamaa ya kujitengenezea fedha ili
kujijengea utajiri.
Watu kama hao
wako tayari kuisaliti nchi kwa kufanya vitendo vinavyoangamiza rasilimali za
taifa ili mradi wanajaza fedha katika makasha yao.
Wapo ambao
kukitungwa sheria za kulinda na kutuza mazingira wao hupiga kofi na kushangiria
mchana, lakini usiku hugeuka wachawi wa kuyaharibu.
Pengine miongoni
mwa waharibifu wakubwa wa mazingira na rasilimali nyengine za nchi kama vile
misitu, bahari na mchanga, ni watendaji wanaopewa dhamana kwa kuaminiwa
kuyalinda ili kuiepusha nchi na janga.
Na haoa ndipo
Muhenga anapoona iko haja kwanza kupambana na TABIA WATU na
baadae tugeukie kulaumu tabianchi, kwa sababu maafa mengi yanayitijkea nchini
chanzo chake ni mikono ya binadamu inayoambatana na utashi wa kujikumbia kila
kitu hata kwa kuwadhuru wengine.
Mathalan, ujenzi
wa miundombinu isiyokuwa na viwango stahili ambayo baaade kuleta
maafa na majanga, chanzo chake ni kugawa zabuni kwa upendeleo na kujuana.
Katika miaka hii
kampuni nyingi za ujenzi pamoja na mafundi binafsi, wanaibuka na kujitangaza
kuwa wao ni mahiri katika kazi hizo na kuomba zabuni mbalimbali.
Kwa bahati
mbaya, mara kadhaa imewahi kuripotiwa wakandarasi kupokonywa kazi walizopewa
kwa mikataba kabla kuzikamilisha baada ya kubainika hazina viwango.
Lakini baya
zaidi, ni pale mkandarasi anapomaliza kazi na kuikabidhi kwa mteja (Hapa
nazungumzia zaidi serikali), lakini baada ya muda mfupi ikadhihirisha ubovu,
huku akiwa ameshatia hasara ya mamilioni kama si mabilioni ya fedha.
Aidha, mara
nyengine miundombinu isiyokuwa imara hutokana na ujanja wa baadhi ya watendaji
wanaoongozwa zaidi na tamaa binafsi, kwa kuwapa kazi waomba zabuni wasiokuwa na
sifa ili mradi wameahidiwa asilimia kadhaa ya fedha.
Ni ukweli usio
shaka kwamba rushwa imekuwa chanzo kikubwa cha matatizo mengi yanayotokea
kwenye miundombinu, na kwa bahati mbaya hata inapobainika hakusikiki hatua
madhubuti zinazochukuliwa ili hali kama hiyo isijitokeze
tena.
Kwa mfano,
ujenzi wa barabara, madaraja, majengo ya taasisi kama vile skuli, hospitali na
ofisi nyengine mbalimbali, umekuwa ukikwangua mno hazina ya serikali huku
thamani ya fedha zilizotumika ikiwa haionekani.
Kupitia tafakuri
hii, Mujega anashauri, ili tuwe na miundombinu imara itakayodumu kwa miaka
mingi na kukomesha maafa yanayoweza kuepukika, ni lazima serikali inoe meno
yake maradufu ili kuwafanya wasimamizi wa shughuli za ujenzi wa majengo na
miundombinu yetu wawajibike ipasavyo.
Aidha mtindo wa
kuchagua washindi wa zabuni za serikali kwa misingi ya usahibu na udugu nao
usipewe nafasi kwani ndio unaosababisha maafa yasiyotarajiwa.
Kwa upande wa
wananchi ambao ndio waathirika wakubwa wa majanga yakiwemo ya kimaumbile, nao
hawana budi kuzingatia maeneo salama ya kujenga nyumba za makaazi na wasiwe
watumwa wa shida walizonazo kwa kujenga popote hata kwenye njia za maji au
mabondeni.
Kwa hakika
ujenzi holela na katika maeneo hatarishi, umekuwa chanzo cha nyumba na majengo
ya taasisi kujaa maji na kuwafanya wakaazi wawe watu wa kuhama na kurudi kila
msimu wa mvua unapofika na kumalizika.
Lakini hili la
ujenzi wa nyumba za makaazi, serikali na Idara zake zisingoje mpaka watu
wamejenga katika maeneo hatarishi kisha kuwabomolea wakati walifuata taratibu
zote za kupata viwanja na vibali vinavyowaruhusu kujenga.
Iwapo inaamua
kuwahamisha watu waliojenga mabondeni au kwengineko kusikoruhusiwa, basi pia
iwawajibishe maofisa wanaobariki ujenzi huo kwa kuwachukulia hatua stahiki.
Halikadhalika,
shughuli za ujenzi zifanyike kwa kutumia wataalamu waliosajiliwa na Bodi ya
Usajili wa Wabunifu na Wakadiriaji wa Majengo badala ya kuachia kila anayeweza
kushika kijiko ajenge.
Ni dhahiri
kwamba kuchukua hatua katika suala hili kutaonesha kwamba kuna mikakati katika
ngazi ya taifa, mkoa, wilaya na shehia inayolenga usimamizi wa kudhibiti maafa
hapa nchini.
Jambo hili ni
changamoto kubwa ambayo inaweza kutatuka endapo kutakuwa na ushirikiano na
uratibu mzuri baina ya wadau mbalimbali.
Simu:
0777865050/0714425556
0 Comments:
Post a Comment