SMZ yaahidi kuimarisha mazingira rafiki kwa wajasiriamali Pemba



Na Amina Ahmed,Pemba

aahmed@marhabanews.net


Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema itaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wajasiriamali kisiwani pemba ili     kukuza biashara zao na kujipatia kipato  .

hayo ameyasema mkuu wa mkoa wa kusini pemba Matar Zahor Masoud katika mafunzo ya ya siku moja ya wajasiriamali yalioandaliwa na benki  kuu  ya Tanzania b o t pamoja  na ofisi ya rais fedha na mipango zanzibar huko katika ukumbi wa ofisi hizo gombani chake chake  pemba.

 Amesema tayari serikali ya Mkoa huo  inaendelea kuboresha  miundo ikiwemo milango  kwa ajili ya Wafanya  biashara itakayosaidia upatikanaji wa soko kwa urahisi kwa wajasiriamali.

Akizungumza katika mafunzo hayo Afisa Mdhamini ofisi ya Rais fedha na mipango  pemba Abdul wahab Said Abuubakar amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwawezesha kielimu wajasiriamali kutunza fedha  na kuweza kuzitumia kwa matumizi yanayotakiwa .

Akiwasilisha mada mchumi muandamizi kutoka bank ya tanzania  B.O.T  Yurick  Mumburi amesema  lengo la kuwekwa mada mbili zinazohusiana na fedha ni kusaidia wajasiriamali hao kujua hali ya uwekaji na uingiaji fedha katika biashara zao.

Nao  washiriki wa mafunzo hayo  wamesema kupitia mafunzo hayo kutawafanya kuweza kufanya matumizi kwa usahihi bila kuziharibu fedha zao ambapo wamesema awali walikuwa wanatumia fedha bila mipango maalum na kurudisha nyuma harakati zao za ujasiriamali. 

Katika mafunzo hayo  ya siku moja mada mbili ziliwasilishwa kwa wajasiriamali hao ni elimu ya fedha  pamoja na usimamizi wa fedha na uwaandaaji wa bajeti.

About mmedia

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment