Jeshi la
Polisi visiwani Zanzibar limetakiwa kuendelea kulinda na kuheshimu kuheshimu
misingi ya haki za binaadamu ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi
Zaidi.
Wito huo
umetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo Cha huduma za Sheria Zanzibar (ZLSC)
Bi Harusi Mpatani wakati alipokuwa akitoa mafunzo ya siku moja kwa askari
polisi juu ya haki za binadamu na umuhimu wa askari polisi kuziheshimu haki
hizo, huko katika ukumbi wa chuo cha Polisi Ziwani, Mkoa wa Mjini MAgharibi
Unguja.
Akiwasilisha
mada ya Misingi ya haki za binadamu na makundi ya haki za binadamu, Bi harusi amewataka
askari hao kuheshimu na kuilinda misingi hiyo katika utendaji wao wa kazi.
Aidha amewataka
kuheshimu mipaka ya utendaji wao wa kazi, kama ilivyoainishwa na katiba ya
Zanzibar na ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yam waka 1977.
“Uniform
na silaha ni dhamana kwenu kwa hivyo hamutakiwi kukiuka sheria na kanuni za
nchi zilizopo”alisema Bi Harusi kuwambia wanafunzi wa jeshi la polisi
Msimamizi
wa mafunzo ambaye ni Mkuu wa utawala wa chuo cha polisi Ziwani, ACP Hasin
Ramadhan Taufiq, akimwakilisha Mkuu wa Chuo ACP Augostino Senga amesema elimu
ya sheria na haki za binadamu ni muhimili muhimu kwa jeshi la polisi katika
kutekeleza vyema majukumu yao ya ulinzi wa raia.
“Sisi
kama jeshi la polisi tunaamini kwamba mafunzo haya yanakwenda kuwa msaada
mkubwa katika utendaji wetu wa kazi” alisema ACP Taufiq.
Washiriki
wa mafunzo hayo ambao ni askari wanaosomea cheo cha ukoplo, wamesema mafunzo hayo
ni mazuri na yatawasaidia sana katika utekelezaji wa mjukumu yao.
Mafunzo
hayo ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya kiutendaji ya kituo cha huduma za
sheria Zanzibar (ZLSC) katika kuhakikisha haki za binadamu zinalindwa kwa
taasisi za serikali na zisizo za kiserikali na hasa kwa wasimamizi wa sheria wa
jeshi la polisi na idara maalum za SMZ.
Amsema
kwa sasa wanatarajia kufikia asakari elfu 3000 ambao watawapatia elimu ya
sheria na haki za binadamu na wapo katika majadiliano kwa upande wa idara
maalum za SMZ ili waweze kuwafikishia elimu hiyo.
Sambamba
na hilo wanaendelea pia kuwafundisha wananchi mbali mbali kupitia vipindi vya
televisheni na redio ili wajuwe umuhimu wa ulinzi wa haki za binadamu Pamoja na
kuheshimu sheria.



0 Comments:
Post a Comment