Na Amina Ahmed
aahmed@marhabanews.net
Jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba limefanikiwa kukamata jumla ya kete 350 zinazodaiwa kuwa ni madawa ya kulevya aina ya heroini sambamba na kuwashikilia watu wengine ambao wanadaiwa kuhusika na biashara hio.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Kusini Pemba ACP Richard Tadei Mchovu amewataja waliokamatwa na madawa hayo
kuwa ni Ali Mjawiri mwenye umri wa miaka 40 mkaazi wa Madungu ambaye alikamatwa
maeneo ya Africana na mwengine ni Said
Moh`d (30) mkaazi wa Minazini Chake Chake ambao wote wawili wamekamatwa kwa
tuhuma za aina moja.
Kamanda huyo pia aliitaka jamii kisiwani humo kutowafumbia macho watu wanaodhani wanahusika na uingizaji,usambazaji n ahata matumizi ya dawa za kulevya na kuwataka kutoa taarifa katika vyombo husika ili waweze kuchukuliwa hatua.
Aidha Kamanda Mchovu
amesema katika operesheni ya usalama barabarani wiki hii jeshi la Polisi Mkoa
wa Kusini Pemba imekamata jumla ya pikipiki 65 kwa makosa mbali mbali ikifemo
kutokuwa na leseni, bima, na makosa ya kutovaa helment kwa madereva na abiria
ambapo baada ya kufikishwa mahakanai
baadhi ya maderva wa vyombo hivyo wamelipa faini na ambapo jumla ya shilingi milioni moja laki
tatu na elfu 20 elfu zimepatikana.
Hata hivyo kamanda huyo
amesema operation hizo mbili ni endelevu ambazo lengo lake ni kumaliza
vitendo viovu katika mkoa huo.
0 Comments:
Post a Comment