![]() |
| Afisi habari wa Afisi ya makamu wa kwanza wa rais Zanzibar Raya Hamad akielezea hatua za kuchukuwa ili kufikia malengo kwa watendaji katika mafunzo yaliofanyika Afisini hapo. |
![]() |
| Mkufunzi wa watendaji wa Afisi ya Makamu wa kwanza wa rais, Ali Sultan akifahamisha jambo wakati mafunzo hayo yaliofanyika leo katika afisi hiyo.( Picha Zote na OMKR) |
Katibu Mkuu Ofisi ya
Makamu wa Kwanza wa Rais Dkt Omar Dadi Shajak amewataka Maafisa Habari wa ofisi
hio pamoja na taasisi zilizo chini yake kuwa wabunifu katika utendaji wao wa
kazi na kutekeleza majukumu yao ipasavyo
Ameyasema hayo wakati
akifungua mafunzo ya siku ya siku mbili kwa Maafisa Habari na tehama wa Ofisi
ya Makamu wa Kwanza wa Rais na taasisi zilizo chini ya Ofisi hio kwenye ukumbi
wa mkutano wa uliopo Migombani, mjini Zanzibar
Dkt Shajak
amewakumbusha Maafisa Habari hao kutumia ujuzi wao na kuhakikisha wanatoa
taarifa sahihi na kwa wakati kupitia tovuti, televisheni, redio, magazeti,
majarida, mitandao ya kijamii
“Mafunzo haya yanayowalenga nyinyi Maafisa
Habari Mawasiliano na Uhusiano muweze kufanya kazi kwa weledi na pia
kujitathmini utendaji wenu kwani nina imani baada ya mafunzo haya kutakuwa na
mabadiliko katika utendaji wenu wa kazi jambo ambalo litawawezesha wananchi
kufahamu majukumu ya Ofisi hii nini tunakifanya, kipi tunakitekeleza na
matarajio yetu
Aidha Dkt Shajak
amewataka maafisa hao vinara katika kutangaza shughuli mbalimbali zinazofanywa
na OMKR wakielewa kuwa majukumu mahsusi ni Kuratibu masuala ya Uendeshaji,
Utumishi na Mipango ya Ofisi, Kusimamia na kuratibu utekelezaji wa masuala yote
ya kisera, mipango ya Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais
Kusimamia masuala ya
Mazingira, Kuratibu na kusimamia masuala ya Ukimwi, Kuratibu masuala ya
Udhibiti wa dawa za kulevya, na Kuratibu masuala ya Watu Wenye Ulemavu ili
wananchi wafahamu maendeleo yanayofanywa na Serikali yao kupitia OMKR.
”Ili majukumu haya
yatekelezwe basi zinazotekeleza sio sera nzuri wala sheria nzuri bali ni
utekelezaji wa zile sera na ile sheria yenyewe na wale wanaotekeleza wanahitaji
taarifa zao si tu kufika kwa walengwa lakini pia kufika zile taarifa sahihi kwa
walengwa na wapelekaji wa taarifa hizo
ni nyinyi maafisa habari ”
Mkurugenzi Uendeshaji
na Utumishi ndugu Juma Ali Simai amesema maafisa habari hawapaswi kuwa nyuma
kutokana na mabadiliko yanayotokea hivyo ni muhimu kupata muda wa kukumbushana
na kufahamu mabadiliko ya ulimwengu ili kwenda sambamba na fani yao
Nae Afisa Habari Mkuu
wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Raya Hamad Suleiman kwa niaba ya Maafisa
Habari wameahidi kutekeleza vyema majukumu yao kwa kuihabarisha jamii na kutoa
ushauri kwani wao ni daraja kati ya Ofisi hio Serikali na wananchi
Wakufunzi wa Mafunzo
hayo ni Mwandishi mwandamizi Ali N. Sultani, muongozaji na mtayarishaji wa
vipindi ndugu Kassim Kh. Jape na Mkuu wa Chuo cha Habari SUZA Bi Imane O. Duwe
Jumla ya mada tano
zimeandaliwa katika mafunzo hayo ya siku mbili zikiwemo Umuhimu wa kuwa Afisa
Habari, kazi na majukumu ya Afisa Habari, Uandaaji wa Documentari, Kuhariri
video na uandishi wa skript, Jinsi ya kuandaa taarifa kwa waandishi na mkutano
na waandishi wa habari pamoja na
Matumizi sahihi ya Teknolojia ya Habari kupitia mitandao ya kijamii


0 Comments:
Post a Comment