Maofisa habari wa afisi Makamu wa kwanza Rais Zanzibar wanolewa


Afisi habari wa Afisi ya makamu wa kwanza wa rais Zanzibar Raya Hamad akielezea hatua za kuchukuwa ili kufikia malengo kwa watendaji katika mafunzo yaliofanyika Afisini hapo.

Mkufunzi wa watendaji wa Afisi ya Makamu wa kwanza wa rais, Ali Sultan akifahamisha jambo wakati mafunzo hayo yaliofanyika leo katika afisi hiyo.( Picha Zote na OMKR)


Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Dkt Omar Dadi Shajak amewataka Maafisa Habari wa ofisi hio pamoja na taasisi zilizo chini yake kuwa wabunifu katika utendaji wao wa kazi na kutekeleza majukumu yao ipasavyo 

 

Ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya siku ya siku mbili kwa Maafisa Habari na tehama wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais na taasisi zilizo chini ya Ofisi hio kwenye ukumbi wa mkutano wa uliopo Migombani, mjini Zanzibar

 

Dkt Shajak amewakumbusha Maafisa Habari hao kutumia ujuzi wao na kuhakikisha wanatoa taarifa sahihi na kwa wakati kupitia tovuti, televisheni, redio, magazeti, majarida, mitandao ya kijamii

 

 “Mafunzo haya yanayowalenga nyinyi Maafisa Habari Mawasiliano na Uhusiano muweze kufanya kazi kwa weledi na pia kujitathmini utendaji wenu kwani nina imani baada ya mafunzo haya kutakuwa na mabadiliko katika utendaji wenu wa kazi jambo ambalo litawawezesha wananchi kufahamu majukumu ya Ofisi hii nini tunakifanya, kipi tunakitekeleza na matarajio yetu

 

Aidha Dkt Shajak amewataka maafisa hao vinara katika kutangaza shughuli mbalimbali zinazofanywa na OMKR wakielewa kuwa majukumu mahsusi ni Kuratibu masuala ya Uendeshaji, Utumishi na Mipango ya Ofisi, Kusimamia na kuratibu utekelezaji wa masuala yote ya kisera, mipango ya Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais

 

Kusimamia masuala ya Mazingira, Kuratibu na kusimamia masuala ya Ukimwi, Kuratibu masuala ya Udhibiti wa dawa za kulevya, na Kuratibu masuala ya Watu Wenye Ulemavu ili wananchi wafahamu maendeleo yanayofanywa na Serikali yao kupitia OMKR.

 

”Ili majukumu haya yatekelezwe basi zinazotekeleza sio sera nzuri wala sheria nzuri bali ni utekelezaji wa zile sera na ile sheria yenyewe na wale wanaotekeleza wanahitaji taarifa zao si tu kufika kwa walengwa lakini pia kufika zile taarifa sahihi kwa walengwa na wapelekaji  wa taarifa hizo ni nyinyi maafisa habari ”

 

Mkurugenzi Uendeshaji na Utumishi ndugu Juma Ali Simai amesema maafisa habari hawapaswi kuwa nyuma kutokana na mabadiliko yanayotokea hivyo ni muhimu kupata muda wa kukumbushana na kufahamu mabadiliko ya ulimwengu ili kwenda sambamba na fani yao

 

Nae Afisa Habari Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Raya Hamad Suleiman kwa niaba ya Maafisa Habari wameahidi kutekeleza vyema majukumu yao kwa kuihabarisha jamii na kutoa ushauri kwani wao ni daraja kati ya Ofisi hio Serikali na wananchi

 

Wakufunzi wa Mafunzo hayo ni Mwandishi mwandamizi Ali N. Sultani, muongozaji na mtayarishaji wa vipindi ndugu Kassim Kh. Jape na Mkuu wa Chuo cha Habari SUZA Bi Imane O. Duwe

 

Jumla ya mada tano zimeandaliwa katika mafunzo hayo ya siku mbili zikiwemo Umuhimu wa kuwa Afisa Habari, kazi na majukumu ya Afisa Habari, Uandaaji wa Documentari, Kuhariri video na uandishi wa skript, Jinsi ya kuandaa taarifa kwa waandishi na mkutano na waandishi wa habari pamoja na  Matumizi sahihi ya Teknolojia ya Habari kupitia mitandao ya kijamii

About mmedia

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment