Na Abdalla Hemed Ali
ahemed@marhabanews.net
Uchakavyu wa majengo na huduma za choo zisizoridhisa
katika kampasi ya Mkuruma chuo kikuu cha Taifa Zanzibar SUZA zinatajwa kuwa changamoto kubwa zinazowakabili wanafunzi
wanaosima katika kampasi hio.
Kutokana na uwepo wa changamoto hio Mkuu wa Wilaya ya Magharib
A Unguja Suzani Kunambi alifika katika
eneo hilo na kuutaka uogozi wa chuo hicho kuhakikisha changamoto hio
inatatuliwa haraka iwezekanavyo.
Alisema Serikali inatambua na kuthamini juhudi za
wanafunzi hivyo kuna kila sababu wanafunzi hao kuwekewa mazingira mazuri
ikiwemo huduma za nzuri za vyoo.
Kwa upande wake mtalamu wa maswala ya afya kutoka chuo
kikuu cha Taifa Zanzibar SUZA Dkt.Hamisa Juma
alisema ni wazi kuwa vyoo vya vinavyotumiwa na wanafunzi katika kampasi
hio si rafika na havipaswi kutumiwa na wanafunzi.
Akizungumzia suala hilo mkuu wa kampasi ya Mkuruma
Dkt,Haroun alisema anafahamu uwepo wa chanagmoto hio na tayari walishamkabidhi
kazi hio mkandarasi lakini hadi sasa hawajui amekwama wapi.
Alisema hata hivyo katika kampasi hio kuna vyoo zaidi
ya hamsini hivyo ni gharama kubwa kukarabati vyoo hivyo na nijambo linalopaswa
kutazwa kwa upana zaidi.

0 Comments:
Post a Comment