CUF Zanzibar waanza mkakati wa kumtoa Lipumba Uenyekiti.

 



 Na Amina Ahmed,Pemba

aahmed@marhabanews.net

Katika hali isiokua ya kawaida wala kutarajiwa na wengi katika medali za kisiasa visiwani Zanzibar na Tanzania kwa ujumla aliekuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wanachi CUF Zanzibar Ndugu Abass Juma Muhunzi amemtaka Mwanyekiti wa chama hicho  Prf,  Ibrahim Lipumba  kujiuzulu  katika nafasi hiyo  mara moja kutokana kile alichokiita  kushindwa kuitendea haki nafasi ikiwa ni pamoja na kukiyumbisha chama hicho kwa upande wa Zanzibar.

 

Akizungumza na waandishi wa Habari  wa vyombo mbali mbali  kisiwani Pemba  Muhunzi alisema  Mwenyekiti wa chama hicho amekuwa mtu wa mwanzo anaevunja katiba ya chama hicho na kujichukulia  sheria mikononi mwake kwa maslahi yake binafsi  bila kuangalia maslahi ya chama hicho jambo ambalo linarudisha nyuma  maendeleo katika chama.

Alisema CUF ni miongoni mwa vyama vilivyoasisiswa kwa malendo maalumu ikiwa ni pampoja na kuwagomboa wananchi kutokana na shida mbali mbali hivyo inapotokea Mwenyekiti kuvunja katika ni sawa na kuipinga dhamira ya kuasisiwa chama hicho.

Alieleza kuwa njia pekee ya kukinusuru chama hicho ni Mwenyekiti wa kuachia nafasi hio ili apishe wengine ambao watakiongoza chama kwa misingi ya katiba.

 

Kwa upande wake Kaimu Makamu mwenyekiti wa upande wa Zanzibar Mussa Haji Kombo alisema endapo  mwenyekiti huyo ataendelea  kubaki katika chama hicho  chama kitazidi kupoteza hadhi yake kwa wanachi kwa vile  kiongozi huyo anasababisha migogoro ya kila siku ndani ya chama hicho pamoja na kukikosesha maslahi muhimu  yakuendeshea harakati za chama.

Alisema njia pekee ya kukiendesha na kukiimarisha chama hicho ni Mwenyekiti kukaaa pembeni ili wenye nia safi waendeshe chama.

Alisema Wanachama wanapaswa kufahamu ukweli juu ya dhamira alionayo Mwenyekiti wao kwa sasa ni pamoja na maslahi binafsi bila kuzingatia maslahi mapana ya walio wengi.

 

 

Kwa upande wake aliewahi kuwa Naibu katibu mkuu Zazibar Ali Makame alisema kuendesha chama bila ya kufuata katiba ni kwenda kinyume ambapo hukumu yake ni kuadhibiwa.

 

Alisema kwa muda mrefu mwenyekiti wao amekua akiendesha chama bila kufuata katiba na kupelekea mgawanyiko mkubwa kwa upande wa Zanzibar na Tanzania bara

 

Mkutano huo wa waliokua viongozi wa CUF ulijumlisha viongozi mbali mbali wapatao 34 kutoka maeneo tofati ya kusini na kaskazini Pemba.

 

About mmedia

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment