Mkurugenzi ZAFELA Jamila Mahmoud Juma akifungua mafunzo ya siku tatu kwa vijana 60 kutoka wilaya zote za Unguja. |
| Fransiska Camilius Clement akichangia kuhusu umuhimu wa wanawake na kushika nafasi za uongozi. |
| Abrahman Sultan Abrahman kutoka ZAFAYCO akichangia mada katika mkutano huo. |
| Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo ya siku tatu wakiendelea kupatiwa elimu. |
Unguja.
Mkurugenzi wa Jumuia ya Wanasheria Wanawake Zanzibar
(ZAFELA )Jamila Mahmoud Juma amesema ipo haja kwa jamii kufahamu umuhimu wa
uongozi bora na demokrasia katika maeneo yao wanayoishi ili kujenga jamii yenye
usawa.
Ameyasema hayoa ofisini kwake kwa mchina mjini Unguja
kufuatia mafunzo ya siku tatu kwa vijana 60 kutoka wilaya zote za Unguja ambao
watakua na kazi ya uhamasishaji katika jamii kuhusu umuhimu wanawake kushiriki
kwenye uongozi na demokrasia.
Alisema kundi hilo la vijana watakua na kazi ya
kuwaelimisha wengine kwenye jamii sambamba na kuhamaisha wanawake kushiriki kwenye
nafasi za uongozi.
Alieleza kuwa kupitia elimu hio anaamini wanawake
wengi watajitokeza kuwania nafasi za uongiozi au hata kuhakikisha wanachagua
viongozi wazuri na wenye manufaa kwa maslahi yao.
Awali mratibu wa mradi wa ushirikishaji wanawake
katika uongozi TAMWA-ZNZ Salma Amir Lusangi
alisema mradi huo unalenga kuwafikia wanawake 6000 ili waweze kudai haki
zao katika uongozi.
Amewataka washirki wa mafunzo hayo waelewe kwamba wana
jukumu kubwa la kuwahamisisha wanawake kudai haki zao za uongozi ikiwemo
kisiasa,kiuchumi na kijamii.
Kwa upande wake Fransiska Camilius Clement alisema
uwepo wa nafasi maalumu za uongozi kwa wanawake ni kitu ambacho hakipasawi
kuondolewa kwa kuwa kunatoa fursa kwa wanawake wengi kujiadaa.
Katika hatua nyengine alisema kuna haja ya jamii
kuwaunga mkono wanawake wanaojitokeza kugombea nafasi mbali mbali za uogozi
kwani wanawake ni watu waliojaaliwa na huruma kuliko wanaume hivyo ni rahisi
kutekeleza majukumu yao.
Mradi huu wa ushirikishwaji wanawake na uongozi unatekelezwa na TAMWA-ZNZ,ZAFELA na PEGAO chini ya ufadhili ya Ubalozi wa Norway Nchini Tanzania na unalenga kuwafikia wanawake 6000 kutoka wilaya 11 za Unguja na Pemba.
0 Comments:
Post a Comment