Watatu wafarikia 28 walazwa Hospital baada ya kula Samaki mwenye sumu Msuka Pembe

Baadhi ya watu walikula nyama ya samaki aina ya Kasa wakikimbilia Hosptali ya Micheweni
 


WATU watatu wamekufa  na wengine zaiidi ya 28 wamelazwa katika Hospitali ya wilaya  Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba wakiendelea kupatiwa matibabu   baada ya kula samaki  aina ya  Kasa mwenye sumu  katika shehiya ya Msuka wilayani humo.

 

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mganga mkuu wa Wilaya hiyo, Dkt. Mkubwa Habibu amesema kwamba  tayari wagonjwa waliofika katika hospitali hiy
o wamelazwa na wanaendelea kupatiwa matibabu chini ya uangalizi wa madaktari huku akibainisha changamoto ikiwa kukosa  ushirikiano pamoja na  taarifa sahihi kutoka kwa waathirika wa tukio hilo.

 

“Wale wote waliopata kula samaki huyo tunawaomba wafike Hosptal mapema ili kupata matibabu ya  haraka” alieleza Mganga Mkuu.

 

Mapema Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya aliyefika katika hospitali hiyo kuangalia maendeleo ya waathirika hao na kuwataka wananchi  waliotumia samaki huyo kujisalimisha  katika kituo cha afya ili waweze kupatiwa matibabu.

Amina Hamad Omar kutoka kijiji cha Tumbe alisema alipelekewa samaki huyo kutoka msuka kwa ajili ya kitoweo.

"nilipika samaki yule mwenye manofu kama ya nyama ya Ng'ombe baada ya kupika, niliwapatia watoto kabla ya mimi, mara watoto wanalalamika mauimivu ya tumbo" alisema Amina

alisema baada ya hapo waliwachukuwa watoto hao na kuwakimbiliza Hospitali ya Micheweni kwa ajili ya matibabu zaidi.

 

Kwa upande Seif Mzee Khamis ni mzazi wa watoto wawili waliofariki kutokana na tukio hilo  amesema 

About mmedia

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment