Na Hassan Mselem,Pemba
hmselem@marhabanews.net
Vijana katika Wilaya ya Chake Chake wametakiwa kuachana na vitendo vya uhalifu na udhalilishaji na badala yake kufanya kazi kwa bidii ili kuzidisha kasi ya maendeleo katika Wilaya hiyo.
Kauli hiyo imetolewa na Afisa mdhamin Wizara ya Habari, Vijana,
Utamuduni na Michezo Salum Ubwa Nassor wakati akifungua mashindano ya mpira wa
miguu yatakayojumuisha timu 16 za Wilaya hiyo, amesema ripoti mbali mbali
zinaonesha kukithiri kwa vitendo vya uhalifu na udhalilishaji visiwani
Zanzibar, hivyo basi amesema kuanzishwa kwa Mashindano hayo yatawasaidia vijana
kujitambua na kuachana na vitendo hivyo.
Ameongeza kuwa ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2021 ibara ya 188 inahimiza
umuhimu wa michezo na sanaa, hivyo basi amewaomba vijana kulitilia mkazo suala
la michezo ili kuhakikisha wanakuwa na afya bora na imara.
Akisoma risala katika ufunguzi wa mashindano hayo mkuu wa jeshi la
polisi Wilaya ya Chake Chake Akama Mohammed Shaaban amesema lengo la kuanzishwa
kwa mashindano hayo ni kupambana na vitendo vya uhalifu katika Wilaya hiyo
kupitia mradi wa polisi jamii wa vijana na michezo.
Mashindano hayo yamejumuisha timu 16 za mpira wa miguu katika Wilaya ya
Chake Chake yameanza rasmi Octoba 4\2021 ambapo timu ya Shamasi Fc na
Chanjamjawiri Fc zilifungua Dimba ambapo timu ya Shamasi Fc iliilaza bao 1 timu
ya Chanjamjawiri Fc bao lililofungwa na Hamad Ali Hamad dakika ya 50, kauli
mbiu katika mashindano hayo isemayo
‘’Chake Chake bila ya
vitendo vya uhalifu inawekana’’.
0 Comments:
Post a Comment