Zoezi la Uhakiki wa Sakata Master Life laanza rasmi Pemba

 



Na - Amina  Ahmed

aahmed@marhabanews.net

Pemba

Jumla ya Mikataba  541 kisiwani Pemba   iliyokusanywa na kampuni ya Master life  kwa upande wa Kisiwani Pemba inatarajiwa  kufanyiwa uhakiki  kwa lengo la kusaidia kupata  fedha na stahiki  zao  kwa wananchi wote walikuwemo katika kampuni hiyo baada ya serikali kusitisha  kuendele kutoa huduma  kwa kampuni hiyo  . 

Akizungumza   katika ukumbi wa  wa Mesi ya Polisi Madungu  Chake Chake Pemba Mkurugenzi  Fedha,  Mipango  Sera  na Utafiti na utafiti  kutoka  Ofisi  ya Rais  Fedha na  Mipango Zanzibar  Saum  khatib  Haji   amesema lengo la  zoezi hilo   limeanza na wananchi wameitikia vizuri wito huo wa kufanya uhakiki  baada ya Serikalii ya Mapinduzi Zanzibar kutoa  agizo la kufanyika kwa uhakiki huo  

 Nae Meneja wa  kampuni hiyo tawi  la  Pemba  Muhammed Abdalla Salum  amesema  itaendelea kusimamia zoezi hilo   litahakikisha kunapatikana takwim sahihi ambazo zitasaidia kupata  stahiki zao kwa kila mwananchi  aliekuwa katika  kampuni hiyo  anapata haki zake kwa mujibu wa sheria. 

Nao baadhi ya wananchi waliojitokeza katika  uhakiki huo  akiwemo  Halima Juma Khamis Na Seif Abass  Ali wamesema matarajio yao ni kuona wanapata haki zao  ambazo waliwekeza katika kampuni hiyo. 

Master life ni kampuni  inafanya  biashara ya fedha  inachukuwa fedha  na kupokea  kutoka kwa wananchi  na kurejesha faida kinyume na taratibu ya biashara  hiyo ambapo  zoezi hilo kwa hapa kisiwani pemba linatarajiwa  kumaliza kesho tarehe saba kwa upande wa kisiwani pemba na serikali ya mapinduzi Zanzibar  ilisitisha shughuli zake na mahkama kutoa uamuzi juu ya kampuni hiyo.

About mmedia

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment