Wizara ya habari Pemba yaahidi kuwafunda vijana na uongozi



Na Amina Ahmed 

aahmed@marhabanews.net

Wizara ya Habari Vijana Sanaa na Michezo imesema itaendelea kuwapa mafunzo ya Uongozi Viongozi wa mabaraza ya Vijana ili kusimamia utendaji   katika  Shehia zao kwa lengo la kuchangua maendeleo kwenye jamii zao.

Afisa Mdhamini wizara ya Habari Vijana Sanaa na Michezo Pemba  Salum Ubwa Nassor ametoa kauli hiyo wakati akifungua mafunzo ya uongozi kwa viongozi mbali mbali wa mabaraza ya Vijana yaliyofanyika Gombani  Kisiwani  Pemba. 

Alisema ipo haja kwa maafisa wa Vijana kuwapa mafunzo ya Uongozi ambayo yataweza kusaidia kuiongoza jamii ili kusaidia kuleta maendeleo katika jamii sambamba na Tifa kwa ujumla. 

Aidha Mdhamini huyo aliwataka  Vijana hao kuwa na mashirikiano kuacha mifarakano isiyo ya lazima ambayo itaweza kurudisha nyuma maendeleo ya mabaraza na   vijana katika shehia  zao

Baadhi ya Washiriki katika mafunzo hayo wamesema mafunzo hayo yataweza kuwasadia kwa kiasi kikubwa katika kusimamia utekelezaji wa majukumu yao kwenye shehia zao.

Mafunzo hayo ya Siku moja ya Uongozi kwa mabaraza ya Vijana yamewashirikisha Viongozi  wakuu  wa mabaraza ya vijana ya shehia  kusini na kaskazini Pemba.


Imehaririwa na Muhammed Khamis

mkhamis@marhabaews.net

About mmedia

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment