Oman kuisaidia Zanzibar kifaa maalumu ya cha kutazamia muandamo wa mwezi

Mufti  wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi,  akimkaribisha Balozi Mdogo wa Oman aliepo Zanzibar Said Salim  Al-sinawiy,  alipofika Ofisi ya Mufti  Mazizini Mjini Unguja  kujitambulisha .



Mufti  wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi akimkaguza baadhi ya vitengo vilivyomo ndani ya Ofisi ya Mufti wakati alipofika kujitambulisha.

Mufti  wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi,  akizungumza na Balozi Mdogo wa Oman aliepo Zanzibar Said Salim  Al-sinawiy alipofika Ofisini kwake Mazizini Mjini Unguja  kujitambulisha.

Balozi mdogo wa Oman aliepo Zanzibar Said Salim  Al-sinawiy akiagana na watendaji wa Ofisi ya Mufti mara baada ya kufika Ofisini hapo na Kujitambulisha .

Na Ali Issa - Maelezo 

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatarajia kupata msaada wa kifaa cha kuangalia  Mwezi mwandamo kutoka  Serikali ya Oman.

Kifaa hicho kinatarajiwa kufika mwaka huu kabla ya mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Hayo yamesemwa leo huko Ofisi ya Mufti wa Zanzibar na Balozi Mdogo wa Oman, Said Salum Al-sinawi alipofika ofisini hapo kujitambulisha kufuatia Balozi aliokuwepo awali kumaliza mda wake.

Amesema Zanzibar na serikali ya Omani ni watu wenye udugu wa damu kwa mda mrefu, hivyo ipo haja ya kuisaidia katika kila nyanja ya maendeleo.

“Mimi naelewa kuwa Zanzibar na Oman ni ndugu wa damu tutakuwa pamoja ili kuendeleza udugu wetu” alisema Balozi huyo. 

Amesema anacho kifanya hivi sasa ni kuangalia maombi yote yaliyofika mezani katika ubalozi huo ambayo yamepangwa kutekelezwa na Balozi aliepita na kuyapa  umuhimu na kuyafanikisha kwani hilo ndio jukumu lake .

“Nimeona maombi yenu mara tu kufika Ofisini ni jambo jema nitashughulikia hilo ni masuala muhimu kuweza kutekeleza”, aliongeza kusema balozi huyo.

Amesema ameyaona maombi yao yapo mezani ikiwemo maombi ya uendelezaji wa ujenzi wa Ofisi ya mufti,kifaa chakuangalizia mwezi na mambo mengine mengi ambayo ni muhimu.

”Nimeona maombi na nitayafanyia kazi na hichi kifaa chakuangalizia mwezi kitafika kabla ya Mwezi mtukufu wa Ramadhani”,alisema Balozi Ali Salum.

Nae Mufti wa Zanzibar sheikh Saleh Omar Kabi, alimshukuru kiongozi huyo kwa ujio wake kufika ofisini hapo na kusema ujio huo ni kuendeleza udugu wao wa damu ambao Zanzibar inafaidika sana na Misaada ya Serikali ya Omani ikiwemi ujenzi wa Misikiti,nyumba za kihistoria,vyuo na maeneo mengine ya kijamii.

Mufti huyo alisema, Omani iendelee kuisaidia Zanzibar na isiishie hapo kwani misaada yao imekua ni chachu ya kuendeleza masuala ya dini ya kislamu katika visiwa vya Zanzibar hivyo ni muhimu sana kuona dini ya kislamu inasimamiwa misingi yake.

Aidha mufti huo alisema kuwa wao wako tayari kuendelea na kuisimamia ofisi hiyo kwa nia safi ili kuendeleza uislamu na kusimamia taratibu zake.

  

About mmedia

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment