Raya
Hamad Suleiman – OMKR
Katibu kuu Ofisi ya
Makamu wa Kwanza wa Rais Dkt,Omar Dadi Shajak
amesema uwepo wa sera na
sheria zinazoendana kati ya Tanzania bara na
Zanzibar ni fursa ya
kuongeza ufanisi na kufikia malengo ya taasisi hizo.
Ameyasema
hayo katika kikao cha mashauriano ya pamoja kati ya Ofisi ya Makamu wa Kwanza
wa Rais
kupitia Baraza la Taifa la Watu wenye Ulemavu na ujumbe kutoka Ofisi ya Waziri
Mkuu
wenye lengo
la kukuza ushirikiano na kubadilishana uzoefu hasa katika sekta ya Watu
wenye
Ulemavu.
Dkt Shajak
amesema katika kukuza ufanisi ni vyema kuimarisha uhusiano wa karibu uliokuwepo
wa taasisi
zote mbili kuzungumza lugha moja ya kiutendaji kwa vile kila upande una
mafanikio
na
changamoto za kiutendaji lakini mwisho wa siku tunazungumzia mafanikio na
maslahi ya
Watanzania
ya Watu wenye Ulemavu.
Naibu
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Profesa Jamal Adam amesema lengo la ujio wao
ni
kujifunza
kutoka pande zote mbili kwa kubadilishana uzowefu na kuangalia miongozo wapi
panahitaji
maboresho pamoja na kupeana mawazo ya kiutendaji.
“leo
tumejifunza utaratibu mzuri uliopo wa kukusanya takwimu za Watu wenye Ulemavu
ambazo
zinakwenda mpaka kwenye Shehia hili tunaondoka nalo na wenzetu wa Zanzibar
tumeona wao
bado hawajawa na vyuo katika stadi za kazi na marekebisho kwa Watu wenye
Ulemavu
hapa tunaona kuwa tumepata kitu kizuri kwa pande zote mbili na tutafanya kazi
kwa
pamoja
“alisisitiza Profesa Jamal.
Mkurugenzi
wa Baraza la taifa la Tatu la Watu wenye Ulemavu ndugu Ussi Khamis Debe
amesema
Baraza la Taifa la Watu wenye Ulemavu na Sekretarieti yake wanashughuli kubwa
ya
kuratibu
masuala ya Watu wenye Ulemavu kwa Serikali na kijamii kwa ujumla.
Nae
Mkurugenzi anaeshughulikia masuala ya Watu wenye Ulemavu kutoka Ofisi ya Waziri
Mkuu ndugu Jacob
Mwinula amesifu uwepo wa mfumo wa kielekroniki ambao unarahisisha
kupata
taaarifa sahihi kwa ajili ya ustawi wa haki za watu wenye ulemavu, pamoja na
suala la
miundo
mbinu ambapo amesema Zanzibar imepiga hatua kubwa hivyo watahakikisha miongozo
hio wanaifanyia
kazi kwa manufaa ya kiutendaji.
Aidha Jacob
amesema Watu wenye Ulemavu wanayo haki na nafasi ya kujiendeleza na kupata
huduma kwa
jamii sawa na watu wasio na ulemavu na kuongeza kuwa ushiriki wao katika
maisha ya
kila siku ndani ya jamii hauna budi kulenga katika kupunguza au kuondosha
maisha
tegemezi
Katika
kikao hicho mapendekezo kadhaa yametolewa ya kukuza ushirikiano ikiwemo kuwepo
ushiriki wa
pamoja kati ya Zanzibar na Tanzania Bara kwenye ushiriki wa mikutano ya
kimataifa
na kikanda.
Kuimarishwa
mashirikiano juu ya utekelezaji wa mikataba ya kimataifa juu ya haki za Watu
wenye
Ulemavu pamoja na kuangaliwa suala la Watu wenye Ulemavu kama ni suala la haki
za
kibinaadamu Tanzania nzima.
Vikao hivyo
ni muendelezo wa mikakati ya serikali katika kuimarisha
utendaji
kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muuungano wa
Tanzania
kwa mambo
yasiyokuwa ya Muungano kwa sekta ya Watu wenye Ulemavu.
0 Comments:
Post a Comment