Dkt,Mwinyi atoa wito kwa wafanya biashara kuacha kupandisha bei za bidhaa

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikata utepe kulifungua jengo jipya la Bodi ya Mapato Zanzibar.(ZRB) lilioko katika eneo la Gombani Wilaya ya Chakechake Pemba na (kulia kwa Rais) Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya (ZRB) Bw.Saleh Sadiq na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar Mhe.Jamal Kassim Ali na (kushoto kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe.Mattar Zahor Masoud.Pica na IKULU





Na Amina Ahmed,Pemba

aahmed@marhabanews.net


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Hussein Ali Mwinyi amewataka wafanya biashara kutopandisha bei za bidhaa   kwani Serikali  imefanya punguzo la kodi kwa lengo la kuwanufaisha wananchi  na wafanya biashara.

Ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi katika ghafla ya ufunguzi wa jengo la  ZRB Gombani Chake Chake Pemba.

Amesema baadhi ya wafanya biashara wanaitumia vibaya  fursa hiyo na kuwazidishia  wananchi gharama za matumizi kutokana na kupandisha bei za bidhaa  hovyo siku hadi siku jambo ambalo   amewataka kuliwacha mara moja kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria.

Hata hivyo  Dk Mwinyi  amebadilisha  k utaratibu wa umiliki wa  mashamba ya eka ya serikali ambapo awali ilikuwa baada ya kufariki baba na mama hurejeshwa serikalini na kupewa watu wengine na kuagiza sasa watoto wapewe mashamba hayo. 

Ziara hiyo katika  wilaya ya chake chake Dk Mwniyi  amepita katika maeneo mbali mbali ikiwemo barabara ya kipapo mgelema, Hospitali ya Chake Chake  ukaguzi wa kisima cha maji chanjaani ambapo  katika maeneo yote hayo  wananchi walipata kuzungumza na rais huyo na kumweleza kero mbali mbali zinazowakabili na kumuomba awasaidie kuzipatia ufumbuzi.

 Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali Mwinyi yupo kisiwani pemba atatimiza siku ya tano katika ziara yake ya kikazi ambapo itamalizia  katika Wilaya Mkoani kwa  kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo katika wilaya hiyo pia atapokea maoni na kero za wananchi wa wilaya hiyo.


About mmedia

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment