| Mkurugenzi wa TAMWA-ZNZ Dkt,Mzuri Issa |
Mkurugenzi Mtendaji wa chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA, Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali amesema vyombo va habari vi apaswa kutenda kazi zake kwa lengo la kujenga uchumi, demokrasia na kutetea makundi muhimu ambayo yako pembezoni.
Kauli hiyo
aliitowa wakati alipokuwa akizungumza na wadau na waandishi wa habari katika
mkutano kwa njia ya zoom ulioandaliwa na TAMWA-Zanzibar na Internews Tanzania.
Alisema kuwa kutokana na umuhimu wa vyombo hivyo, mara
nyingi makundi mbalimbali yakiwemo ya wanasiasa hujaribu kufanya mbinu nyingi
za kuvidhibiti vyombo hivyo.
“Mkusanyiko huu ni
muhimu sana kwetu hivyo ni vyema waandishi wa habari wapaze sauti zao kwa
kuleta maslahi na sio kuleta mifarakano,’’alisema.
Akitowa mada ya
changamoto ya vyombo vya habari mwakilishi kutoka PPC Ali Mbarouk Omar
aliwataka waandishi wa habari kupaza sauti zao zitakazotatua migogoro ya jamii
na kuifanya kuwa na mshikamano na maamuzi sahihi.
Nae Rashid Omar
alisema aliwataka waandishi kuandika habari zao kwa kutumia maadili ya kazi
zao, ili kuondokana na changamoto mbalimbali zinazowakabili.
Wakitowa ushuhuda
wa changamoto zilizowahi kuwakumba katika kazi zao mwandishi Haji Nassor wa
gazeti la Zanzibar leo na Rahma Suleiman wa Nipashe waliwataka waandishi wa
habari wasirudi nyuma wanapopata vitisho katika kazi zao.
Akichangia mada
mwandishi mkongwe Salum Vuai alisema viongozi watakapozidisha ushirikiano na
kuacha kuwabana waandishi wataweza kufanya kazi zenye kuleta mafanikio kwa
jamii husika.
Watoa mada Ali
Mbarouk Omar, Rashid Kombo na Shifaa Said Hassan, wamewaka waandishi hao
kutokuwa karibu mno na vyanzo vyao vya habari, kama hali hiyo itatishia kazi
yao.
Shifaa alisema,
jambo la kwanza kwa waandishi wa habari kuhakikisha habari zao wanazoziripoti
zinawasaidia wananchi wa kawaida.
Akifunga mkutano
huo, Mkufunzi mwandamizi kutoka shirika la habari la Intarnews Tanzania Alakok
Mayombo alisema ipo haja ya kurekebisha baadhi ya sheria za habari kwani
zinaonekana kubana uhuru wa habari na utendaji wa kutumikia umma.
Alifahamisha kuwa
Tanzania na Visiwani wameridhia mkataba wa haki za binadamu hivyo kuna haja ya
sheria hizo kukaa sawa, ili habari ziweze kupatikana kama inavyostahiki.
“Kazi ya
uchehemuzi itakapofanywa kwa kiwango husika lengo la kupatikana uhuru wa habari
litafanikiwa ,“alisema.
Alieleza kuwa ni jambo lisilopingika kuwa kunyima uhuru wa habari ni kunyima
haki za binadamu na kuleta uwajibikaji usiofaa.
“Unapoandika
habari kwa wakati itasaidia kutoa maamuzi yatakayoleta maendeleo hivyo
linalowezekana leo lisingoje kesho”,alisema.
Mkutano huo
uliowashirikisha wadau wa habari na waandishi wa vyombo mbalimbali nchini ni
ushirikiano kati ya chama cha waandishi wa habari, Zanzibar Tamwa na shirika la
Intanews Tanzania.
0 Comments:
Post a Comment