Messi amwaga machozi akiaga Barcelona

 Nahodha wa FC Barcelona Lionel Messi hatimae leo afanya mkutano Nou Camp kwa ajili ya kuwaaga rasmi viongozi, wachezaji wenzake pamoja na mashabiki.

“Mkataba wangu haikuwa ishu sana ninachokijua ni kwamba nilifanya kilaninaloweza kufanya ili nibaki (Barcelona), club ilishasema hilo haliwezi kutokea sababu ya LaLiga”>>>> Messi

“Naweza kukuhakikishia kuwa nilifanya kila ninaloweza ili kubakia lakini haikuwezekana, kweli mwaka uliopita sikutaka kubaki (Barcelona) na nililisema hilo ila mwaka huu ilikuwa ni tofauti nilitaka kuendelea”>>> Messi

Messi (34) ameitumikia FC Barcelona karibia kipindi chote cha maisha yake, alianza kuichezea timu za vijana za Barcelona toka 2003 alipojiunga nayo akitokea Newell’s Old Boys ya kwao Argentina na 2004 ndio akaanza kucheza timu ya wakubwa ya Barcelona

About Marhaba

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment